Fahari ya Serengeti

Sunday, September 17, 2017

WAKAZI WA ITUNUNU SERENGETI WAPAZA SAUTI KUKATAA UKEKETAJI



Mwenyekiti wa Muungano koo ya Inchage Sungura Mturi akitoa tamko la kupiga marufuku ukeketaji kwa wakazi wa Itununu wilaya ya Serengeti ikiwa ni makubaliano ya wazee wa mila wa koo sita wilayani humo kutokomeza ukeketaji kwa watoto wa kike baada ya kupata elimu sahihi ya madhara ya ukeketaji.
Wazee wa mila ambao ndiyo walikuwa vinara wa kusimamia ukeketaji kwa madai ya kutimiza mila na desturi,sasa ni vinara wa kuelimisha jamii kwa kupitia koo zao ,na kuwa watu watakaokaidi watashughulikiwa kwa misingi ya mila na desturi na sheria kwa kuwa zama zimebadilika.

Makubaliano yao ya kutokomeza Ukeketaji yametiwa saini na wazee wa mila wa koo zote mbele ya Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurdin Babu ,Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti unaotekelezwa na amref health africa,Kituo cna Sheria na Haki za Binadamu(LHRC)Halmashauri na wadau wengine chini ya Ufadhili wa UN WOMEN.

Mwaka jana baadhi ya wazee wa mila na ngariba walinaswa na polisi baada ya kujihusisha na ukeketaji na baadhi wamefungwa na wengine kesi zinaendelea mahakamani .

 Wazee wa mila wa koo ya Inchage wakiwa kwenye kikao katika kijiji cha Itununu
 Wananchi wakifuatilia mkutano wa wazee wa mila




 Inspekta wa Polisi Alfred Malimi akitoa msimamo wa serikali kwa watakaokaidi maagizo ya wazee wa mila
 Wasanii wa Nuru Sanaa wakitoa elimu kwa wakazi wa kijiji cha Itununu
 Elimu kwa njia ya Sanaa

0 comments:

Post a Comment