Fahari ya Serengeti

Thursday, September 28, 2017

ILI KUPANDISHA HADHI ZAHANATI YA BUSAWE,HALMASHAURI YATAKIWA KUKAMILISHA UJENZI WA WODI

 Halmashauri ya wilaya ya Serengeti imetakiwa kutoa fedha za ujenzi wa wodi zahanati ya Kisaka na kukamilisha baadhi ya majengo ili kuiwezesha serikali kuipandisha hadhi na kuwa Kituo cha Afya.
Naibu Waziri wa Afya Dk Hamisi Kigwangala amesema kufanya hivyo kutakuwa kumeongeza maeneo maalum ya kutolea huduma za afya kwa wananchi wake.
"Wakazi wa hapa waishio nje wamejitahidi sana kwa ujenzi wa zahanati hii ili kuhakikisha wananchi wa maeneo haya wanapata huduma za afya karibu ,halmashauri kazi iliyoko mbele yenu ni kutoa fedha za kukamilisha baadhi ya miundo mbinu ili iweze kupandishwa hadi,"amesema.
Mapema kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo William Makunja amesema wametenga sh 24 mil kupitia mapato ya ndani ili kusaidia ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali.

 Diwani wa kata ya Busawe Ayobu Makuruma akielezea walivyofanikiwa kujenga zahanati hiyo na mikakati yao ya baadae





0 comments:

Post a Comment