Fahari ya Serengeti

Saturday, December 31, 2016

WAZUIA MSAFARA WA NAIBU KWA MABANGO

Wakazi wa Kijiji cha Nagusi wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara wamezuia msafara wa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhandisi Ramo Makani wakiwa na mabango yenye ujumbe wa tembo,Njaa na kuwasilisha kilio chao,hata hivyo amekiri kuwa wakazi wa wilaya hiyo wanapata madhara makubwa kutokana na tembo  ikifuatiwa na Bunda.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhandisi Ramo Makani akikagua shamba la mtama la  Mkazi wa kijiji cha Singisi kata ya Nagusi wilayani Serengeti Gitang'ita Komesha lililoliwa na Tembo usiku wa kuamkia desemba 31 ,2016,amekiri kuwa wilaya ya Serengeti inaongoza kwa athari zinazosababishwa na tembo .
NaibuWaziri akijadiliana na madc wa Serengeti na Bunda baada ya kuwasili eneo la Tirina wilayani Serengeti

Ukaguzi Shambani ukiendelea
Mwenye shamba Komesha akieleza madhara aliyokwishapata toka mwaka 2014 mpaka sana ,hajawahi kuvuna wala kifuta jasho hajawahi pata licha ya kujaza fomu.
Mjadala shambani unaendelea
Hatimaye wakaendelea
Ilibidi wapitie ramani kuona ulipo mpaka wa hifadhi na makazi ya wananchi,hata hivyo imebainika licha ya kuwa mbali na hifadhi haijasaidia kutopata madhara.
Wakazi wa Singisi wakazua msafara wa waziri kwa mabango.
Mbunge wa Jimbo la Serengeti Marwa Ryoba akaeleza jinsi tembo wanavyochangia umaskini wa wakazi wa wilaya hiyo kutokana na kula mazao yao,hawana chakula.



Maneno yakamwingia
Ziara ikamfikisha kwenye mji wa mkazi wa Makundusi ambaye nyumba yake iliezuliwa na tembo kisha akala chakula kilichokuwa ndani.


Mwenyekiti wa halmashauri Juma Porini akionyesha teknolojia ya kuzuia tembo iliyobuniwa na wananchi baada ya kukosa msaada wa wizara ya wanyamapori.

Askari wako imara kwa bosi wao.
Dc Nurdin Babu akasema wilaya imeishawasilisha taarifa kwa Mkuu wa Mkoa kuomba chakula cha msaada maana wakulima wamelima lakini hawavuni sababu ya tembo
Afisa wanyamapori wilaya John Lendayan akitoa taarifa ya madhara ya tembo na mikakati ya wilaya,hata hivyo amesema hali ni mbaya kunatakiwa mikakati ya haraka ili kunusuru wananchi.
Ziara ikawafikisha ofisi ya Senapa Fort Ikoma iliyoungua moto


Hatimaye wakapeana mikono ya kwa heri baada ya kuhitimisha ziara.
Wakati wa maswali waandishi hawakusita kumuuliza naibu waziri ,kwanini wanatenga fedha za kulipa waliokufa,kujeruhiwa  na mazao badala ya kuzielekeza kwenye ulinzi,amesema wizara itafanyia kazi eneo hilo kwenye mipango yake.
Hatimaye safari ya kuelekea Mwanza ikaanza.

Thursday, December 29, 2016

WANALAANI UKEKETAJI




BODABODA KIJIWE MAMA MUGUMU WACHANGIA DAMU

 Bodaboda wa Kijiwe Mama Mjini Mugumu wilayani Serengeti wakipata maelezo toka kwa kaimu mratibu wa damu salama Jamhuri Kabati umuhimu wa kuchangia damu na hitaji lake katika hospitali Teule ya Nyerere .
 Wannashiriki kufanya usafi kabla ya kuchangia damu
 Usafi unaendelea
 Wanajioroshesha



 Kamanda Pareso naye ni miongoni mwa wadau wa uchangiaji damu
 Wakitoka hospitali baada ya kuchangia unit 28 za damu
 Baada ya kuchangia soda zilinyweka
 Anachangia damu

Wednesday, December 28, 2016

BUSAWE SERENGETI WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO

Diwani wa Kata ya Busawe wilayani Serengeti Mkoa wa Mara Ayubu Makuruma kushoto akitoa ufafanuzi wa miradi waliyotekeleza bila fedha ya serikali ikiwemo ujenzi wa Kituo cha afya na vifaa vyake chenye thamani ya zaidi ya sh 200 mil,ujenzi wa ofisi ya kijiji na kata yenye thamani ya zaidi ya sh 30 mil.miradi ya elimu na maji kwa kutumia wazawa wa kijiji na kata hiyo walioko nje ya wilaya na mkoa wa Mara,kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo Nurdin Babu
Wazawa wa kijiji cha Busawe kata ya Busawe wakiwa pamoja na viongozi wa kijiji,kata na wilaya ya Serengeti wakijadiliana mambo mbalimbali kabla ya kazi ya kukagua miradi na harambee ya kuchangia ujenzi wa nyumba ya Mwalimu shule ya msingi Bisawe.
Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurdin Babu akiwa na viongozi wenzake wakati wakielekea kwenye chanzo cha maji katika kijiji cha Busawe.
Safari inaendelea.
Akina mama nao walikuwepo


Dk James Mataragio Mkurugenzi wa TPDC ambaye ni mzawa wa kijiji cha Busawe akihamasisha wenzake namna ya kuchangia miradi ya maendeleo ili kuwapunguzia adha wananchi .
Uzinduzi wa Ofisi ya Kijiji iliyojengwa kwa nguvu za wananchi ukifanywa na Dc Nurdin Babu
Tunakata utepe anasisitiza Dc Nurdin Babu
Kama ilivyo ada wanasaini kitabu cha wageni
Ded Serengeti Mhandisi Juma Hamsini kushoto anatoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ambayo halmashauri yake imepanga kutekeleza kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2016/17
Dc akiongoza harambee ambapo zaidi ya sh 15 mil zilichangwa kati ya lengo la sh 24 mil kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu.