Fahari ya Serengeti

Monday, February 9, 2015

PICHA ZA MATUKIO YA WATU WALIOKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUMFICHA KIJANA MMOJA KISHIRIKINA ROBANDA SERENGETI

 Moja ya nyumba ya mtuhumiwa wa uchawi ikiwa imeteketezwa kwa moto na wananchi na mikoba yote ikaungulia mle
 Jumla ya nyumba saba ziliteketezwa kwa moto na wananchi ,ikiambatana na kipigo kwa watuhumiwa watatu.,
 Watu mbalimbali walifika eneoe la tukio
 Wananchi wakiwa eneo la tukio wakifuatilia maombi kwa kijana Matiko Mkeya(20)aliyekuwa ametoroshwa na kufichwa bafuni kwa mmoja wa tuhumiwa akiwa amefungwa sanda na hana fahamu.
 Wakazi wa kijiji cha Robanda wakifuatilia tukio hilo la aina yake kutokea eneo hilo.
 Wanafuatilia.
 Maombi ndani yanaendelea ili kuvunja nguvu za pepo hatimaye kijana akapata ufahamu na kurudia hali ya kawaida.
 Wengine walikuwa na silaha kama inavyoonekana hapo
 Watumishi wa Mungu wanazidi kushusha upako kwa kijana aliyekuwa amegeuzwa Zombie na hatimaye Mungu akatenda miujiza na kuvunja nguvu za shetani
 Mambo yanaendelea taratibu

 Kijana aliyekuwa amegeuzwa Zombie mara baada ya kupata ufahamu,alichukuliwa feb.7 saa 3.usiku akiwa amelala,alipatikana feb 8 majira ya saa 6 bafuni kwa mmoja wa watuhumiwa akiwa amefungwa sanda nyeupe ikiwa imeandikwa namba 7 kwa rangi nyekundu.
 Kijana Matiko akiwa amepata fahamu huku akiwashangaa watu waliojumuika

 Kijana akiwa amekaa huku akiwashangaa watu muda mfupi baada ya kupata fahamu.

 Anadai yeye anakumbuka alivyokuwa amelala wakaingia watu wakamwambia siku hiyo ndiyo mwisho wake kwa kuwa anajifanya mlokole ,na wamemsaka kwa muda mrefu kutokana na kujidai kwake kuwanyima maziwa.
 Baadhi ya nyumba za watuhumiwa zikiteketea kwa moto




 Ramadhani Chibagi maarufu kama Chatu Mkali akwia kituo cha polisi ni miongoni mwa watuhumiwa watatu wa tukio la uchawi.
 Watuhumiwa wa uchawi kutoka kulia Chatu Mkali katikati mkewe Chausiku Juma na kushoto ni Ghati ambaye alitajwa na Chausiku kuwa ni miongoni mwa mtandao wao,wakiwa kituo cha polisi Mugumu Serengeti
Kijana alikutwa ndani ya bafu la Chatu Mkali na mkewe Chausiku ambao wanadaiwa kusumbua wananchi kwa tuhuma za uchawi .

0 comments:

Post a Comment