Fahari ya Serengeti

Sunday, September 17, 2017

SERENGETI BILA UKEKETAJI SASA YAWEZEKANA,SASA NI KUSOMESHA MTOTO WA KIKE KWA KASI KUBWA

 Meneja wa Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti unaotekelezwa na amref health africa,LHRC,Halmashauri na wadau wengine chini ya Ufadhili wa UN WOMEN ,Godfrey Matumu wa tatu toka kulia akiwa na wazee wa mila wa koo ya Inchugu kata ya Machochwe kwenye eneo lao mahsusi kwa ajili ya vikao vya mila kijiji cha Nyamakendo kabla ya kuanza mkutano uliotishwa na wazee wa mila ili kutoa tamko la kupiga marufuku ukeketaji kwa watoto wa kike na kuhimiza kuwasomesha.

Misimamo hiyo ya wazee ni dalili ya Nuru njema kwa watoto wa kike na kudhihirisha kuwa Serengeti bila ukeketaji inawezekana
Walipo wazee wa mila Mradi wa Tokomeza Ukeketaji unawafikia kama inavyoonekana hapo kwenye eneo maalum la kikao cha wazee wa koo ya Inchugu(Wakira)

0 comments:

Post a Comment