Fahari ya Serengeti

Thursday, September 28, 2017

JELA MIAKA 10 KWA KUKUTWA NA VIPANDE 7 VYA NYAMA YA NYUMBU

Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara imewahukumu washitakiwa wawili kwenda jela miaka 10 ama kulipa faini ya sh 5mil kwa kukutwa na vipande saba vikavu vya nyumbu vyenye thamani ya sh 1.4 mil.

Akitoa hukumu Hakimu Amalia Mushi amesema washitakiwa Magasi Metache Nyantito(31)wa Parknyigoti na Thomas Ng'ora Mrengi(22)mkazi wa kijiji cha Miseke ambaye hakuwepo Mahakamani baada ya kuruka dhamana,amesema washitakiwa wametiwa hatiani kwa makosa matatu waliyoshitakiwa nayo.

Ambayo ni kukutwa ndani ya hifadhi,kukutwa na silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kumiliki nyara za Taifa vipande saba vikavu vya nyumbu kinyume cha Sheria.

Hata hivyo amesema mlango wa rufaa uko wazi kama hawataridhishwa na maamzi hayo na mshitakiwa amepelekwa gerezani.

0 comments:

Post a Comment