Fahari ya Serengeti

Saturday, September 30, 2017

MRADI WA TOKOMEZA UKEKETAJI SERENGETI WAWAKUMBUKA WAHUDUMU WA AFYA VIJIJINI

 Meneja wa Maradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti Godfrey Matumu kulia akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurdin Babu msaada wa baiskeli na vifaa vingine vya kazi kama mabegi,tisheti na kofia  ukiwa na thamani ya sh 34 mil,kwa ufadhili wa UN WOMEN ,kwa ajili ya Wahudumu wa Afya vijijini ambao wanaelimisha jamii mambo mbalimbali ya afya ikiwemo kupiga vita vitendo vya ukeketaji.
Mradi huo unatekelezwa na shirika la amref health africa,Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC)Halmashauri na wadau wengine.

 Dc Nurdin Babu kushoto akimkabidhi Mhudumu wa Afya Vijijini Julius Antony Baiskeli na vifaa vingine kwa ajili ya kuendeleza kazi za utoaji elimu na kupinga ukeketaji wa watoto wa kike.
 Nakukabidhi baiskeli uitumie kwa kazi kusudiwa isiwe ya kusombea mkaa na vimoro,dc anasisitiza.
 Dc anamkabidhi kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Serengeti Deo Kisaka vifaa hivyo ili aweze kuwapa wahudumu wa afya vijijini.

 Kila mmoja na mchuma wake kwa ajili ya kuingia kazini
 Picha ya Pamoja ilipigwa








 Katibu Tawala wilaya ya Serengeti Cosmas Qamara akisisitiza uwajibikaji wa wahudumu wa afya vijijini

 "Nendeni mkasaidie jamii hasa wajawazito na watoto wakike wasikeketwe,"anasema Dc





0 comments:

Post a Comment