Fahari ya Serengeti

Thursday, June 30, 2016

WAJITOLEA KUJENGA BWENI ;KUWANUSURU WASICHANA RING'WANI SEKONDARI-SERENGETI

 Ctherine Ruge Katibu wa shirika lisilo la Kiserikali la Girls Education Support Initiatives (gesi)kushoto akiwa ameshikana mkono na baba yake mzazi Ruge na wananchi wa kata ya Magange na Ring'wani wakimpongeza kwa uamzi wake wa kusaidia watoto wa kike katika shule ya sekondari ya Ring'wani  wilayani Serengeti,shirika hilo limeanza ujenzi wa bweni la wasichana 56 ili kuwanusuru na adha wanazopata katika maisha ya upangaji kijijini,kazi hiyo itashirikisha mchango wa jamii.
 Mapokezi ya vifaa yalishirikisha viongozi wa kada mbalimbali.


WADAU WAAMUA KUJENGA BWENI KUNUSURU WASICHANA NA MIMBA,
Serengeti Media Centre.
Ili kuwanusuru wanafunzi wa shule za sekondari na mimba,utoro na ndoa za utotoni zinazoendelea wilayani hapa Mkoa wa Mara shirika lisilo la kiserikali la  Girls Education Support Initiatives(gesi)limeanza  kujenga bweni la wasichana katika sekondari ya Ring’wani.
Inadaiwa wasichana zaidi ya 36 wamekatishwa masomo wa sekondari na shule za msingi wilayani hapa wamekatishwa masomo kutokana na ujauzito,pia ndoa za utotoni na utoro huku ukosefu wa mabweni ukitajwa kama chanzo cha tatizo.
Katibu Mtendaji wa shirika hilo lenye makao makuu yake wilayani hapa Catherine Ruge alisema wameanza ujenzi wa bweni litakalosaidia watoto wa kike 56 ambao wamepanga kijijini hapo katika mazingira yanayochangia kukata tamaa ya kusoma.
“Watoto wamepanga kijijini hali inayowafanya waishi maisha kama ya unyumba,wengine wanatoka mbali kiasi kwamba hawahudhurii masomo kwa wakati,waanza wengi wanamaliza wachache na hawafanyi vizuri,ndiyo maana tukatafuta watu wa kutusaidia ili kuwanusuru watoto wa kike,”alisema.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Elibariki Mwita alisema shule hiyo inahudumia kata mbili za Ring’wani na Magange na wengi wanatoka mbali ,wanalazimika kupanga mtaani na wengine wanatembea umbali mrefu hali ambayo inawafanya waache masomo.
“Kwa kipindi cha miaka 13 wasichana 3 pekee ndiyo waliofaulu kwenda kidato cha tano,mwaka 2013 tulipokea wasichana 37 kuanza kidato cha kwanza,lakini waliopo sasa ni 20 pekee ,wasichana 9 wameacha shule  ,wawili wamerudia kidato cha pili na uhamisho wasichana watano,ukosefu wa bweni ni tatizo kubwa hapa kwa kuwa maisha ya mtaani huwageuza kuwa wake za watu,”alisema.
Na kuwa katika mitihani ya majaribio ikiwemo ya BRN wasichana wote hakuna aliyefaulu chanzo kikiwa ni ukosefu wa mabweni.
Ruge akizungumzia mkakati wao alisema ujenzi huo wanategemea kukamilika mwishoni mwa mwaka huu,”inagharimu zaidi y ash 85 milioni kama hakuna nguvu za wananchi,lakini kwa kushirikisha wananchi ambao wamekubali kuchangia nguvu kazi tunategemea kazi hiyo itagharimu zaidi y ash 50 milioni,”alisema.
Alisema shirika lao linalolenga kumsaidia mtoto wa kike wilayani humo lina malengo ya kusaidia shule mbalimbali kadri wanavyopata msaada,aliomba wadau wengine kuwekeza kwenye elimu kama njia pekee ya kumkomboa mtoto wa kike anayekabiliwa na vikwazo vingi ikiwemo mila na desturi.
Diwani wa kata ya Magange George Mahemba alisema kupitia msaada huo wananchi wamekubali kuchangia ili kuwanusuru watoto wa kike .
Mwisho.

 Catherine akiwa na wazazi na baadhi ya viongozi wa kijiji na kata ya Ring'wani na Magange baada ya mtoto wa kike kujitokeza kuwasaidia wadogo zake ili waweze kupata mazingira mazuri ya kuishi na wasome.








0 comments:

Post a Comment