Fahari ya Serengeti

Friday, June 24, 2016

MBUGE YA KUANGAMIZA GUGU LA KIDUHA YAANZA KUSAMBAZWA KWA WAKULIMA WA MAHINDI SERENGETI

Mratibu wa Kampuni ya African Agricultural Technology Foundation (AATF)yenye makao makuu yake  jijini Nairobi  Nchini Kenya na Ofisi ndogo jijini Mwanza, Jovita Joachim wakati wa sherehe ya Mkulima katika kijiji cha Rung’abure  ,akielezea madhara ya gugu la Kiduha linavyoathiri kilimo cha zao la Mahindi wilayani humo.


MBEGU KINZANI ZASAIDIA KUTOKOMEZA GUGU LA KIDUHA,
Serengeti Media Centre Media.
Wakulima wa kata nane wilayani hapa wameanzisha kampeini ya kutokomeza gugu hatari la Kiduha ambalo limekuwa likiathiri uzalishaji wa zao hilo la chakula na biashara.
Kata hizo ni pamoja na Rung’abure,,Manchira,Morotonga,Nyamoko,Uwanja wa ndege,Geitasamo,Mbalibali na Machochwe.
Gugu hilo ambalo inadaiwa kusambaa kwa kasi na kuathiri ukuaji na uzalishaji wa zao la mahindi ,inadaiwa mbegu zake hukaa chini kwa zaidi ya miaka 15 bila kuota na limeathiri wakulima katika nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania.
Akitoa ufafanuzi wa kampeini hiyo Mratibu wa Kampuni ya African Agricultural Technology Foundation (AATF)yenye makao makuu yake  jijini Nairobi  Nchini Kenya na Ofisi ndogo jijini Mwanza, Jovita Joachim wakati wa sherehe ya Mkulima katika kijiji cha Rung’abure jana ,alisema kutokomezwa kwa gugu hilo kutaongeza uzalishaji na kipato kwa wakulima.
“Gugu la Kiduha ni hatari sana maana mche mmoja huzalisha mbegu 40 hadi 50 milioni ,na husambaa kwa njia nyingi ikiwemo mifugo,watu na wakati mwingine upepo…na limechangia wakulima wengi kukata tamaa kutokana na uzalishaji mdogo wanaopata,”alisema.
Alisema baada ya utafiti wa makampuni mbalimbali duniani ulibaini mbegu ya (Meru IR621)ina uwezo wa kutokomeza gugu hilo kutokana na viwatilifu vyake na huongeza uzalishaji  mahindi  kwa ekari moja hadi  magunia 24 kwa kuwa inaua nguvu ya gugu hilo ambalo hufyonza maji chini ya mmea na uharibu rutuba ya ardhi.
Baadhi ya Mikoa ambayo imeathiriwa na gugu hilo ni pamoja na Tanga,Pwani,Lindi,Mtwara,Dodoma,Iringa,Mbeya,Ruvuma,Mwanza na Mara ,na kwa kanda ya ziwa wilaya za Serengeti,Butiama,Musoma,Rorya,Misungwi,Magu,Kwimba,Bunda,Rorya na Butiama.
Kwa Upande wake Mkuu wa wilaya hiyo Maftah Ally aliwataka wakulima kuacha kilimo cha  mazoea na kwa kutumia teknolojia hiyo watafanikiwa kutekeleza kampeini iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa huo Magesa Mulongo ya kujilisha mwenyewe.
“Hakuna haja ya kuhitaji msaada wa chakula kwa wakazi wa wilaya hii kwa kuwa mvua toka agosti mwaka jana hadi sasa inanyesha,tumieni teknolojia ya kisasa ili muongeze mavuno na soko lipo kwa kuwa kuna viwanda vya kusaga unga vinafunguliwa wilayani humo,”alisema.
Akizungumzia mafanikio ya teknolojia hiyo Tatu Nyamuronga mkulima kutoka kijiji cha Miseke alisema yeye ameweza kupata magunia 27 kwa ekari moja ,wakati awali alikuwa akivuna magunia 5hadi 7.
Naye Magoiga Nyamuhanga mkulima kutoka Rung’abure alishauri elimu itolewe zaidi kwa kuwa wakulima  walikuwa wakitilia shaka mbegu kutoota.
Mwisho.


Baadhi ya maafisa wa kilimo wakielezea athari ya gugu la kiduha kwa zao la mahindi.

Baadhi ya wakulima wakiangalia mahindi katika moja ya shamba la mkulima wa kijiji cha Rung'abure.
Burudani mbalimbali zilikuwepo ikiwemo chakula na vinywaji.
















0 comments:

Post a Comment