Fahari ya Serengeti

Thursday, June 30, 2016

KATA YA KYAMBAHI WILAYANI SERENGETI YAVUKA LENGO KATIKA KUCHANGIA MADAWATI

 Afisa Mtendaji wa kata ya Kyambahi wilayani Serengeti Mkome Manyanya akitoa ufafanuzi wa hitaji la madawati kwa sule tatu za msingi katani hapo ambapo madawati yaliyokuwa yakihitajika ni 174 yenye thamani ya zaidi sh 2 mil.lakini  katika harambee hiyo iliyoendeshwa na Mwenyekiti wa Manispaa ya Musoma William Gumbo kwa niaba ya Mbunge wa jimbo la Musoma Mathayo Manyinyi na kupata zaidi ya sh 5 milioni.


MIFUGO ICHANGIE MAENDELEO YA WATOTO KIELIMU,
Serengeti Media Centre
Jamii ya wafugaji wilayani hapa Mkoa wa Mara inatakiwa kubadili mitizamo kwa kutumia rasilimali walizonazo kusomesha watoto wao hasa wa kike badala ya kuwaoza.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti Juma Porini alisema hayo wakati wa harambee ya kuchangia madawati katika kata ya Kyambahi kwa ajili ya shule za msingi tatu zinazokabiliwa na upungufu wa madawati 174.
Alisema sekta ya mifugo inahitaji wasomi na wataalam mbalimbali ambao watasaidia sekta hiyo kutoa matunda mazuri,lakini baadhi ya   wafugaji  wameshindwa kuwekeza kwenye elimu ya watoto wao ambao watasaidia kusukuma maendeleo ya taifa.
“Wazazi hakuna sababu ya kuwatupia lawama walimu juu ya kutofaulu kwa watoto kwenye  masomo yao,chanzo ni ninyi wenyewe kutokuona umuhimu wa kuchangia elimu na kuwaendeleza watoto,kuendelea na tabia hiyo kutalikosesha taifa wasomi …wafugaji utajiri wenu wa mifugo utumike kuleta mabadiliko kwenye familia zenu na jamii ,wekezeni kwenye elimu ndiyo faida isiyokwisha thamani,”alisema.
Akiongoza harambee hiyo iliyolenga kubata madawati 174 yenye thamani ya zaidi ya sh 2 milioni, na kufanikiwa kupata sh 5,124.200 ikiwa fedha taslimu sh3031200, ahadi sh2,093,000,  madawati 105 ahadi ngombe 3,mbuzi 4,Meya wa Manispaa ya Musoma William Gumbo alisisitiza wananchi kuwa mstari wa mbele kuchangia maendeleo yao.
“Ni wajibu wa wazazi kuandaa watoto wao kielimu ili waweze kupata mwanga wa kusaidia jamii,hakuna mtu atakuja kuwasomeshea watoto wenu hilo ni jukumu la kila mzazi,kwa kufanya hivyo mnawaandaa pia kuja kuwa wazazi bora,”alisema.
Gumbo pamoja na kuchangia madawati 10 na kuwasilisha mchango wa madawati 50 ya mbunge wa Musoma mjini Vedastus Mathayo ambaye amewekeza katika kijiji hicho,aliwataka kuachana na dhana potofu kuwa serikali itafanya kila kitu kwa msingi wa elimu bure,bali wazazi wanawajibu pia.
Mapema Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kyambahi Mukome Manyanya na Mratibu elimu kata Nemes Sianga wakitoa taarifa zao walisema mbali na upungufu wa madawati kata hiyo haina shule ya sekondari hali inayochangia utoro kwa kuwa baadhi ya wanafunzi wanatembea zaidi ya saa 4 kufika shuleni.
Walisema moja ya mkakati walionao kwa kushirikisha jamii ni kujenga shule ya sekondari ili kuwapunguzia safari ndefu wanafunzi,hali ambayo pia itachangia mazingira rafiki ya kusoma.
Ili kuhakikisha wilaya hiyo inakamilisha upungufu wa madawati zaidi ya 14,000 kwa shule za msingi na sekondari ,kila kata imepewa jukumu la kutatua matatizo yaliyopo,na wilaya inawaongezea kila kata madawati 20.
Mwisho.

 Baadhi ya viongozi wa kata,tarafa,kijiji na wilaya wakiwa wamekaa wakisubiri utaratibu.



 Mwenyekiti wa Manispaa ya Musoma William Gumbo akiwa anafungua baadhi ya michango ya wadau wa maendeleo wa ndani na nje ya kata hiyo ambapo yeye na mbunge wa Musoma mjini walichangia madawati 60.
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti Naomi Nnko akisisitiza umuhimu wa jamii kuchangia shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

0 comments:

Post a Comment