Fahari ya Serengeti

Friday, June 17, 2016

UKEKETAJI WA WATOTO WA KIKE NGARIBA NA WAZEE WA MILA KUKAMATWA.

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Maftah Ally akitoa onyo kwa ngariba na wazee wa mila watakaojihusisha na ukeketaji wa watoto wa kike mwaka huu,na kuwa watakamatwa na kushitakiwa kwa mjibu wa sheria zilizopo ,amewataka watafute njia nyingine za kujipatia mapato kuliko kutegemea mapato yanayotokana na vitendo vya ukatili kwa watoto wa kike,amewataka viongozi wa vitongoji,vijiji,na kata kuhakikisha wanasimamia agizo hilo na ambaye itatokea eneo lake kunafanyika ukeketaji atawajibishwa.
 Baadhi ya wasichana waliokimbia kukeketwa na kuhifadhiwa katika Nyumba Salama wakionyesha igizo maalum juu ya athari za ukeketaji wa watoto wa kike kiafya,ksaikolojia,kielimu na kiuchumi wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto Afrika kiwilaya katika kijiji cha Nyamoko.


 Wanafuatilia michezo na hotuba
 Wanafunzi wa shule za msingi Nyamoko na Itununu  wakifuatilia michezo na hotoba mbalimbali kutoka kwa viongozi wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika.
 Mambo yanaenda yakiongezeka kutokana na burudani na jumbe mbalimbali zilizotolewa na wanamichezo na viongozi mbalimbaliwa serikali na kisiasa.Jumbe mbalimbali zilitolewa .

 Wanafuatilia michezo mbalimbali katika uwanja wa Nyamoko ikiwa ni katika kuhitimisha kilele cha siku ya mtoto wa Afrika.
 Mkuu wa wilaya akikagua timu kabla ya kuanza michezo.

 Wanafuatilia michezo mbalimbali.

 Diwani viti maalum Esther Nyamhanga akiwaasa wazazi kusomesha watoto wao hasa wa kike na kuachana na vitendo vya kuwakeketa kwa kuwa madhara yake ni makubwa sana .

 Michezo ilikuwa sehemu ya kufikisha ujumbe.



 Wanafunzi wakiimba nyimbo mbalimbali za kuitaka jamii iepuke vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwemo suala la ukeketaji kwa watoto wa kike.
Mkuu wa wilaya ya Serengeti Maftah Ally akikagua timu ya wasichana wa shule za Nyamoko na Itununu ikiwa ni katika kuhitimisha kilele cha siku ya Mtoto kiwilaya katika kijiji cha Nyamoko.

0 comments:

Post a Comment