Fahari ya Serengeti

Sunday, June 12, 2016

TAMASHA LA UIMBAJI KUPINGA VITENDO VYA MAUAJI YA WATU WENYE UALIBISM MUGUMU SERENGETI.

Meneja wa NMB Tawi la Mugumu wilayani Serengeti William Bajunana ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la waimbaji Mugumu lililoshirikisha vikundi mbalimbali,kwaya za waimbaji wakiongozwa na Mwimbaji kutoka Kanisa la KKKT Angaza Igoma jijini Mwanza Lucy Haruni.



WAIMBAJI WA KWAYA WAJITOSA KUPIGA VITA MAUAJI YA WATU WENYE UALIBINISM
Ukosefu wa elimu na hofu ya Mungu ni chanzo cha watu wengi kujihusisha na matendo ya ukatili ikiwemo mauaji ya watu wenye Ualibism katika maeneo mengi hapa nchini.
Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Mugumu wilayani hapa Mkoa wa Mara William Bajunana akiongoza watu kuchangia fedha na vitu mbalimbali kwa ajili ya watu wenye  Ualibinism wakati wa Tamasha la Uimbaji kwenye viwanja vya kanisa Katoliki Mugumu,alisema vitendo hivyo vinachafua sifa ya taifa na mikoa ya kanda ya Ziwa.
Bajunana ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha hilo lililoandaliwa na Mwimbaji kutoka Kanisa la KKKT Angaza Igoma jijini Mwanza Lucy Haruni kwa ajili ya kutafuta fedha ya kuwanunulia pikipiki watu wenye Ualibinism ili iwasaidie kupata kipato,alisema pamoja na kuwa wilaya ya Serengeti haijawahi kukumbwa na matukio kama hayo,lakini picha ya nchi ni mbaya kutokana na matendo hayo.
“Kila mmoja anatakiwa kuguswa na tatizo hili ambalo limechangia wenzetu wenye ulemavu wa ngozi kuuawa kwa misingi ya imani ya kishirikina,na hili ni tatizo kubwa la wananchi wasiopenda kufanya kazi kupata vipato vyao badala yake wanajiingiza kwenye mambo ambayo kimsingi hayana ukweli,tunahitaji kumhusisha Mungu zaidi ili kuvunja nguvu ya shetani,”alisema.
Alisema Kampeini hiyo inayofanywa na watumishi wa Mungu kwa nyimbo inatakiwa kuungwa mkono zaidi ili watu waweze kubadilika kwa kupitia mahubiri ya kwaya,”naomba kila mmoja alione hili kama janga maana hawa ni ndugu zetu hawakupenda kuzaliwa hivi,”alisema.
Akizungumzia lengo la Kampeini hiyo Lucy Haruni alisema nikupata fedha za  kuwanunulia pikipiki moja  watu wenye Ualibinism ili iwasaidie kuingiza kipato kwa kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi,”kwa kuwa tatizo hili si la dhehebu moja ndiyo maana nimeshirikisha madhehebu mengi kwa kuwa hii ni vita na inagusa uumbaji wa Mungu,”alisema.
Katika Tamasha hilo jumla ya zaidi y ash 2.5 milioni ikiwa ni fedha taslimu na ahadi zilitolewa,huku Bajunana pamoja na kuchangia sh 1 mil,akiahidi kuwa kupitia Benki ya NMB kwenye kitengo cha Jamii waombe ili waweze kusaidiwa.
Mwisho.





Paroko wa Kanisa Katoliki Mugumu Alois Magabe akifungua tamasha hilo kwa maombi









Watu wengi walishiriki katika tamasha hilo wakiwemo watoto kama inavyoonekana hapa.




0 comments:

Post a Comment