Fahari ya Serengeti

Saturday, June 18, 2016

MBARONI KWA KUMNAJISI MWANAE WA MIAKA 2,


   



Serengeti Media Centre.
.
Mkazi mmoja wa Kitongoji cha Nyansarari kijiji cha Masinki kata ya Magange wilayani hapa Mkoa wa Mara Mangure Chacha(40)anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumnajisi  mtoto wake wa miaka miwili.
Polisi wilayani hapa ,uongozi wa kijiji na afisa mtendaji wa kata hiyo Ngeya Alfred wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo,ambalo ni lapili  kutokea katika kata hiyo ambapo Mei 25 mwaka huu  mkazi wa kijiji cha Magange   Chacha Kisamo(35)alimbaka mtoto wa miaka 13 na kumsababishia maumivu na kukamatwa kisha kufikishwa mahakamani,hata hivyo mtuhumiwa yuko nje kwa dhamana.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Masinki Maitari Hunda akiongea na Serengeti Media Centre  kwa njia ya simu alisema kuwa tukio hilo linadaiwa kutokea usiku wa kuamkia 14 mwaka huu nyumbani kwa mtuhumiwa ,ambaye kabla ya kufanya unyama huo alimpiga mke wake na kumfukuza nyumbani kwake.
“Baada ya kupata taarifa tulifuatilia nyumbani kwa mtuhumiwa na kumkuta mtoto amelala kitanda cha baba yake  huku ameumizwa…tulipomuuliza mtuhumiwa ambaye alionekana kulewa alidai hajui na wala hajatenda,lakini anakiri kuwa alilala na  mtoto,”alisema.
Hata hivyo Mama mzazi wa mtoto Christina Joseph(19)alisema juni 13 majira ya saa 2 usiku mme wake alifika akiwa amelewa na kuanza kumshambulia huku akimwapia kuwa atamuua kwa kuwa hafanyi kazi za nyumbani kwake kama anavyotaka.
“Toka juni 11 mwaka huu ilikuwa ni kipigo tu kwangu au kwa mtoto huku akisisitiza kuniua,na juni 13 hali ilikuwa mbaya zaidi,nikaamua kukimbia na kulala kwa mke mdogo wa Mwenyekiti wa kijiji,mtoto wangu alikuwa amelala ndani ya nyumba ya mama mkwe…nilipotoka akamfuata na kuja kulala naye ndipo akamfanyia ukatili huo,”alisema na kuongeza.
“Saa 12 alfajiri nilirudi nyumbani na kumkuta mtoto amelala kitandani uchi,wakati mimi nilimwacha akiwa amevaa,aliponiona akawa anashika sehemu za siri huku analia ,kumwangalia nikakuta ameingiliwa maana mbegu za kiume zikiwa zimetapakaa nje na damu ikivuja,nikatoa taarifa kwa majilani kisha ofisini na kumkamata mtuhumiwa,”alibaisha.
Hata hivyo alimpompeleka mtoto wake zahanati ya Masinki kwa ajili ya kupata matibabu,alikataliwa kwa madai kuwa lazima aende na fomu ya Polisi(PF3),masharti ambayo yalimshinda kutokana na umbali,hata hivyo polisi kupitia dawati la jinsia waliingilia kati kwa ajili ya kusimamia matibabu ya mtoto huyo.
Alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusiana na kiini cha mgogoro huo alikiri kuwepo kwa muda mrefu toka mwaka 2011 baada ya kumuoa akiwa mke wa pili akimdai kuwa hazai,”baada ya mgogoro huo niliondoka na kwenda kwetu nikakaa kwa muda na kupata mtoto,wazazi wake na wa kwangu wakaniambia nirudi ,naye akakubali tukawatunaishi vizuri,lakini akaanza kubadilika taratibu,”alisema.
Mtoto na Mama watoroshwa kupoteza ushahidi.
Katika Mazingira ya kutatanisha Christina akiwa na mtoto aliyenajisiwa na baba yake ametoroshwa na ndugu wa mtuhumiwa ili kupoteza ushahidi wa tukio hilo.
“Polisi baada ya kufika waliuliza mtuhumiwa nikawaonyesha wakaanza kumhoji,wakauliza mama na mtoto walipo ili waweze kuchukua taarifa kabla ya kuondoka,niliwajibu yupo kwa kuwa nilijua hayuko mbali,nikatuma mgambo wamwite,hata hivyo hakupatikana na kuibua wasiwasi kwa wananchi,”alisema Mtendaji wa kijiji.
Hata hivyo aliambiwa na wananchi kuwa mama huyo ameonekana akipanda boda boda akiwa na mwanae na shemeji yake ambaye ni mdogo wa  mtuhumiwa wakaelekea Sirori Simba,hali iliyowalazimu kufuatilia kwa gari.
“Tulifanikiwa kumpata bodaboda aliyewabeba akasema kuwa alikodiwa kuwapeleka hadi Sirori Simba na kuwaacha hapo ambapo walionekana kukodi pikipiki kuelekea Buhemba wilaya ya Butiama,kwa ujumla tukio hilo limeacha maswali mengi lilivyotokea maana kutoroshwa kwa mama na mtoto wamepoteza ushahidi,”alisema.
Alipoulizwa mikakati iliyokuwa inaendelea kabla ya kutoroshwa kwa mama na mtoto,alidai kuwa ndugu walikuwa wakizunguka ofisini hapo wakionyesha wazi kujadiliana na mama wa mtoto kila wakati,na inadaiwa kuna kaka yake na mtuhumiwa aliyeko Bunda ndiye anadaiwa kuratibu zoezi zima la kuwatoroshwa baada ya kutuma fedha kwa ndugu zake kijijini hapo.
Mkuu wa wilaya Maftah Ally alisema mtuhumiwa bado anashikiliwa na polisi na kuhusu mama na mtoto wake wanaendelea kusakwa ikiwemo na wale waliohusika kuwatorosha.
Mwisho.


0 comments:

Post a Comment