Fahari ya Serengeti

Thursday, November 30, 2017

WAZIRI AZINDUA UANDAAJI MPANGO WA MATUMIZI BORA YA ARDHI WILAYA YA SERENGETI

 Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akielezea umuhimu wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi kwa vijiji .mji na Taifa wakati akizindua Uaandaji wa Mpango wa wa Matumizi Bora ya Ardhi wa wilaya ya Serengeti ambao unafadhiliwa na Serikali ya Ujermani kupitia Benki ya Maendeleo ya Watu wa Ujermani na Frankfurt Zoological Society(FZS) kwa zaidi ya sh 63 bil,kwa vijiji 40 wilaya za Serengeti na Ngorongoro,kati ya hizo sh 1.3 bil zitatumika kwa ajili ya Mpango bora wa Matumizi ya Ardhi na nyingine kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mara Kigoma Malima akielezea jinsi Mkoa ulivyojipanga kwa ajili ya kuhakikisha vijiji vingi vinapima ardhi kwa kutumia upimaji shirikishi.
Waziri anakabidi vifaa vya kazi kwa timu ya inayoshiriki zoezi hilo ambalo linafanywa na Frankfurt Zoological Society(FZS)Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Halmashauri ya wilaya ya Serengeti kwa ajili ya kuleta maendeleo na uhifadhi wa Ikolojia ya Serengeti.

0 comments:

Post a Comment