Fahari ya Serengeti

Saturday, November 11, 2017

CHANGAMOTO ZA ELIMU ZAIBULIWA NA RIPOTI YA TWAWEZA BUTIAMA

 Akizindua Ripoti ya Utafiti ya mwaka 2015  iliyofanywa na Twaweza chini ya Mpango wa Uwezo Mratibu wa Mradi huo wilaya ya Butiama  Apaisaria Kiwori amesema,walibaini  asilimia 22 ya wanafunzi wa darasa la saba hawawezi  kusoma hadithi ya Kiswahili ya darasa la pili.

“Asilimia 38 ya wanafunzi wa darasa la saba hawawezi  kufanya hesabu za darasa la pili,huku asilimia 80 ya wanafunzi wa darasa la tatu hawawezi kufanya hesabu za darasa la pili,asilimia 9 ya wanafunzi wa darasa la tatu wanaweza kusoma hadithi za kiingereza ya darasa la pili,na asilimia 33 wanaweza kusoma hadithi ya Kiswahili ya darasa la pili,”alisema.
 Wanafunzi wa shule za msingi Butiama wakifuatilia taarifa ya uzinduzi wa ripoti ya utafiti

 Wanaimba shairi

0 comments:

Post a Comment