Fahari ya Serengeti

Tuesday, November 28, 2017

9 WAFUNGWA KWA MAKOSA YA KUKUTWA NA NYARA ZA ZAIDI YA SH 107 MIL

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara imewahukumu kila mmoja miaka 20 washitakiwa 9  katika kesi nne tofauti baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ismael Ngaile ametoa hukumu hiyo baada ya kuridhishwa na ushahidi wa upande wa Jamhuri ambao ulikuwa ni pamoja na vielelezo kama meno ya tembo,mafuta ya Simba,Mikia ya Nyumbu,na silaha za jadi Sime,pinde ,mishale na nyaya za kutegea wanyama.

Mwendesha mashitaka wa Jamhuri Emmanuel Zumba amesema makosa hayo yalitendeka kati ya mwaka 2016 na mwaka huu,na kuomba mahakama itoe adhabu kali kwa kuwa vitendo hivyo ni vya uhujumu uchumi.

0 comments:

Post a Comment