Fahari ya Serengeti

Tuesday, November 28, 2017

SIKU 16 ZA KUPINGA UKEKETAJI WANAFUNZI SERENGETI WAFUNGUKA KUPINGA UKEKETAJI.

 Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Serengeti Maria Mchala akiwajengea uwezo wa kujitambua na kujisimamia katika maamzi  wanafunzi wa Kisangura sekondari ili kuepukana na vikwazo vinavyoweza kusababisha wasifikie ndoto zao kielimu kama mimba,ukeketaji na ndoa za utotoni.
Katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia wilayani hapo,wadau mbalimbali na wanaharakati wamekutana na wanafunzi wa sekondari Kisangura kwa ajili ya kufikisha ujumbe unaolenga kuleta mageuzi makubwa ya kifkra.
Hata hivyo wanafunzi hao wamesema kuwa ukeketaji ni kikwazo kikubwa kielimu na wanatumia elimu yao kuelimisha jamii ili iweze kuachana na ukatili huo wa kijinsia.

 Wanafunzi wanafuatilia mjadala

 Afisa Vijana wilaya ya Serengeti akitoa mada.
 Meneja wa Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti toka amref health africa Godfrey Matumu akibainisha ukubwa wa tatizo la ukeketaji kiafya na kisaikolojia.
Tunasikiliza

0 comments:

Post a Comment