Fahari ya Serengeti

Wednesday, November 22, 2017

ALAMBA MIAKA 20 KWA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO

MIAKA 20 JELA KWA KUKAMATWA NA MENO YA TEMBO

 Zakaria Wambura(52) Mkazi wa Kijiji cha Nyansurura wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara  amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kukutwa na meno mawili ya tembo yenye thamani ya Tsh 22.5 milioni.

Akitoa hukumu katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 106/2016,Hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya Ismael Ngaile amesema  mshitakiwa atatumikia kifungo cha miaka 20 kutokana na kosa hilo,ambalo ni kinyume na kifungu cha 86 cha Sheria Namba 5 ya Wanyamapori ya mwaka 2009.

Mapema Mwendesha mashitaka wa Jamhuri Emmanuel Zumba ameiambia Mahakama kuwa  mshitakiwa huyo alikamatwa oktoba 29,2016 ndani ya Pori la Akiba la Grumeti,akiwa na kisu,Shoka ,Panga na meno mawili ya Tembo kinyume cha Sheria.

Ameomba Mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa kuwa wanyama hao wako hatarini kutoweka,huku mshitakiwa akiomba mahakama kumpunguzia adhabu kwa kuwa ni kosa lake la kwanza.

0 comments:

Post a Comment