Fahari ya Serengeti

Wednesday, November 22, 2017

VIPANDE VYA NYAMA YA NYUMBU VYA MPELEKA GEREZANI MIAKA 20

MIAKA 20 KWA KUKUTWA NA NYAMA KAVU ZA NYUMBU



Mwita Mwikwabe Chacha (42)mkazi wa kijiji cha Machochwe wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kukutwa na vipande 70 vya nyama kavu ya nyumbu vyenye thamani ya zaidi ya Tsh 56.8 milioni.

Katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 63/2016 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya Ismael Ngaile ametoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo za kuhujumu mali za Umma.
Mapema Mwendesha Mashitaka wa Jamhuri  Emmanuel Zumba mbele ya Hakimu Ismael Ngaile amesema kuwa ,aprili 15,2016 mshitakiwa alikamatwa nyumbani kwake Machochwe akiwa na nyara hizo kinyume cha Sheria.


0 comments:

Post a Comment