Fahari ya Serengeti

Thursday, January 8, 2015

Ahadi ya ujenzi barabara Serengeti yakwama




 Na Mussa Juma, Mwananchi

Posted  Alhamisi,Januari8  2015 
KWA UFUPI
NI ile yenye urefu wa kilomita 421 iliyopaswa kujengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya Sh648 bilioni.
Arusha, Ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Mto wa Mbu, wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha hadi Nata, wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara umekwama baada ya Serikali kushindwa kutoa fedha kama ilivyoahidi awali.
Serikali iliahidi kujenga barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 421 kwa gharama ya Sh648 bilioni, huku eneo linalokatiza ndani ya hifadhi lenye kilomita 53, likitarajiwa kujengwa kwa changarawe.
Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Arusha, Deusdedit Kakoko alisema pamoja na kwamba Serikali haijatoa fedha hadi sasa, ahadi ya kujenga barabara hiyo iko palepale.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Jowika Kasunga wakati akizungumza kwenye Kikao cha Bodi ya Barabara Arusha kilichofanyika juzi.
“Ni kweli ujenzi wa barabara haujaanza, lakini ahadi ya kuijenga iko palepale, kinachosubiriwa ni fedha kutoka Serikali Kuu,” alisema Kasunga.
Awali, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ngorongoro, Elias Ngolisa alihoji lini barabara hiyo itaanza kujengwa kutokana na umuhimu wake.
Ngolisa aliitaka Serikali kueleza kwa nini haijatoa kiasi cha fedha za awali za ujenzi huo, kiasi cha Sh7 bilioni.
“Pamoja na fedha hizo kutotolewa hadi sasa, bado kiasi hicho ni kidogo, labda kitumike kukarabati na siyo kujenga,” alisema.
Ahadi ya ujenzi huo ilitolewa na Rais Jakaya Kikwete ili kuwapunguzia usumbufu wakazi wa Arusha na Mara kutokana na mikoa hiyo kutounganishwa kwa barabara ya lami.


Monday, January 5, 2015

WENYEVITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO WA MUGUMU WAAPISHWA




 BAADHI YA WENYEVITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO WA MUGUMU WILAYA YA SERENGETI WAKIJAZA FOMU ZA VIAPO VYAO
 TARATIBU ZINAENDELEA
 BAADHI YA VIONGOZI WA VYAMA WALISHIRIKI KUSHUHUDIA ZOEZI LA UAPISHAJI
WANASAINI VIAPO
 HAKIMU WA MAHAKAMA YA MWANZO MUGUMU SERENGETI IRONI PONELLA AKITOA MAELEKEZO YA KUZINGATIA KABLA YA KUWAAPISHA
 WANASOMA KAMA WAMEANDIKA VIZURI

 WANAAPA KUWA WATIIFU NA WAAMINIFU IKIWA NI PAMOJA NA KUTUNZA SIRI ZA SERIKALI.
 ISHARA YA KUANZA KAZI
 KIAPO KINAENDELEA

 WENYEVITI 23 WAMEAPA KUMI CCM,CHADEMA 10 NA CUF 3
 MWENYEKITI WA MTAA WA BOMANI NAYE ANAAPA




 WANAWASILISHA FOMU ZA VIAPO MARA BAADA YA KUSAINI
MWANASHERIA WA HALMASHAURI HIYO TUMAINI NYAMHOKYA AKIKUSANYA FOMU ZA VIAPO ILI ZISAINIWE NA HAKIMU

Sunday, January 4, 2015

UMOJA WA MADHEHEBU WAZIKUTANISHA KWAYA MBALIMBALI KUSHEREHEKEA MWAKA MPYA

 KWAYA YA KANISA LA KMT MUGUMU WILAYA YA SERENGETI IKIHUBIRI KWA NJIA YA KUIMBA WAKATI WA IBADA YA UMOJA WA MADHEHEBU KWA AJILI YA IBADA YA MWAKA MPYA ILIYOFANYIKA KATIKA KANISA KATOLIKI
 MWAKA YA KMT
 KWAYA YA BIKRA MARIA MTOTO WA MUNGU KANISA KATOLIKI MUGUMU WAKIIMBA
 KWAYA YA ANGLIKANA WAKIIMBA
 KANISA LA ANGLIKANA




 KWAYA YA MTAKATIFU FRANSISCO WA ASIZI KANISA KATOLIKI MUGUMU

 KWAYA YA  AIC MUGUMU

Saturday, January 3, 2015

MWENYEKITI AWASHANGAZA WENGI AANZA KUTEKELEZA AHADI KABLA YA KUAPISHWA

 FUNDI WA TANESCO WILAYA YA SERENGETI AKIENDELEA NA SHUGHULI ZA KUSAMBAZA NYAYA ZA UMEME  KATIKA KITONGOJI CHA CHAMOTO MAMLAKA YA MJI WA MUGUMU,IKIWA NI UTEKELEZAJI WA AHADI YA MWENYEKITI WA KITONGOJI HICHO JOSEPH RHOBI MAGOIGA(CUF) ALIZOTOA WAKATI WA KAMPENI ZA SERIKALI Z MITAA,UTEKELEZAJI HUO UMEANZA IKIWA NI SIKU 15 BAADA YA KUCHAGULIWA NA HAJAAPISHWA,
 MWENYEKITI WA KITONGOJI HICHO JOSEPH MAGOIGA AMBAYE PIA NI MWENYEKITI WA CUF WILAYA AMETUMIA ZAIDI YA SH 3.5 MILIONI KWA AJILI YA KUNUNUA NGUZO 15 AMBAZO ZITATUMIKA KUSAMBAZA UMEME ENEO HILO AMBALO LICHA YA KUWA MAMLAKA YA MJI LAKINI HAWAKUWAHI KUPATA NISHATI HIYO HUKU WAKIDAI WALIISHI KWA AHADI ZA VIONGOZI.
 KAZI INAENDELEA NA UMEME UNATARAJIWA KUWASHWA JANUARI 15 MWAKA HUU.
 ANASAIDIANA NA MAFUNDI
 BAADA YA KUKAMILIKA KWA KUWEKA UMEME AHADI YA PILI NI KUWASAMBAZIA MAJI WAKAZI WA KITONGOJI HICHO ,ANASEMA WANANCHI WANATAKIWA KUTOFAUTISHA UONGOZI WA CUF NA CCM KWA KUWA WAMEISHI KWA AHADI MUDA WOTE ,LAKINI WALIPOMCHAGUA AMEANZA UTEKELEZAJI.








MKAKATI WA KUMTETEA DED WAWAGAWA MADIWANI

.

 
Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara
wamegawanyika huku kundi kubwa likipinga mpango wa kumtetea aliyekuwa Mkurugenzi wa halmashauri aliyevuliwa madaraka kwa kushindwa kusimamia uchaguzi wa serikali za mitaa.

Uteuzi wa Goody Pamba ulitenguliwa Desemba 17  mwaka huu na  Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Tamisemi)Hawa Ghasia  baada  ya  Rais Jakaya Kikwete kuridhia watendaji wote waliohusika kuvuruga uchaguzi

wachukuliwe hatua.

Baadhi ya madiwani wakiongea na Serengeti media Centre wamesema  hawakubalini na mpango unaoendeshwa na Mwenyekiti wa halmashauri wa kumtetea Pamba kwa madai kuwa kufanya hivyo ni kupingana na uamzi wa Rais Kikwete kwa kuwa
kutofanyika kwa uchaguzi siku iliyopangwa kumechangia kuleta matokeo mabaya kwa CCM katika maeneo mengi.

“Mpango huo hatutakubaliana nao kwa kuwa hauna maslahi kwa wilaya bali kikundi cha watu wachache ambao wanahofu kuondolewa kwake mambo yao mengi yatajulikana….maana alikuwa na kikundi cha madiwani wachache na
watumishi aliowaona bora ,kukaa vikao kwa ajili ya jambo hili ni matumizi mabaya ya fedha za wananchi”anasema diwani mmoja jina tunalo.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo John Ng’oina anasema  kuwa watakaa wajadili kisha nao watoe kauli kuhusiana na uamzi huo ambao anadai haukumtendea haki Pamba kwa kuwa hakuhojiwa na mamlaka zake za
uteuzi ili ajitetee.

“Huyu mama ameonewa maana hajahojiwa sehemu yoyote…hakuna
aliyemlalamikia,baada ya kutokea dosari aliahirisha kwa mjibu wa
sheria na kupanga tarehe nyingine,sasa kutengua uteuzi wake katika
mazingira haya lazima nasi kama halmashauri tulijadili kisha nasi
tutoe sauti yetu”alisema.
Hata hivyo katika kikao cha kamati ya madiwani ya Mipango ,uchumi na
fedha kilichokutana desemba 23 mwaka huu hakikufikia uamzi baada ya
hoja hiyo kuleta mgongano,huku wengine wakitaka waliokuwa wasimamizi
wasaidizi wa uchaguzi nao wachukuliwe hatua.
Katika kikao cha desemba 30 bado hawakupata muafaka na kukubaliana uchunguzi ufanyike utakaofanywa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ili kubaini watumishi wengine waliohusika kuvuruga uchaguzi huo,waweze kuchukuliwa hatua.

“Kuna watu waliokuwa wananufaika kwa tenda na kupitishiwa fedha kwa
ajili ya mambo yao kwa kivuli cha safari za halmashauri ndiyo wako
mstari wa mbele kutaka wote tuungane nao….hili jambo limesababisha
madhara makubwa kidemokrasia,na kwasasa wananchi wanafuatilia kwa
karibu mambo yanayoendelea na fedha zao zinavyotumiwa,”anasema diwanina kuongeza.

“Kuna mkakati wa kuchota fedha baadhi ya watu waende Dar es salaam ama Dodoma kumtetea ,hizo ni fedha za wananchi ambazo zingesaidia kwenye ujenzi wa vyumba vya maabara ama kulipia karo watoto

watakaokosa karo…. Matendo kama haya yataendelea kututesa kwa
jamii,”anasema.

Habari kutoka kwa chanzo kingine kilisema kuwa baada ya kusikia Rais
Kikwete alipokuwa  kwenye mapumziko ya sikukuu  katika hotel ya Four Session  ndani ya hifadhi ya Taifa yaSerengeti ,wanasiasa walitumwa  ili arudishiwe madaraka,hata hivyo hawakufanikiwa.
Mmoja wa watu ambaye anadaiwa kuwa na uhusiano wa karibu na mkurugenzi aliyevuliwa madaraka na pia mnufaika wa zabuni kwa kofia ya nafasi yake ndani ya Chama hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo baada ya mkakati wake kukataliwa.

Hata hivyo baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa vinavyounda Ukawa
wilayani hapa walisema kuwa uamzi wa kumvua madaraka ulikuwa sahihi
kutokana na uzembe wa kufanya maandalizi ya uchaguzi,huku wakidai kuwa katika vikao vyao vyote aliwahakikishia kuwa maandalizi yamekamilika,wakati hali ilikuwa kinyume.
Wanasema kuwa hapakuwa na maandalizi ya kutosha kwa kuwa hata baada ya kuahirisha uchaguzi  bado vifaa vilipungua na kulazimisha watendaji kuwa wanatoa nakala  karatasi za kupigia kura kwenye maduka,huku matukio ya watu kukamatwa na  karatasi za kupigia kura yakijitokeza.
Mwisho.