Fahari ya Serengeti

Monday, August 31, 2015

WENYE USHAHIDI WA UFISADI WA LOWASSA WAWEKE HADHARANI-



Paroko wa kanisa Katoliki Mugumu wilaya ya Serengeti Alois Magabe akiendesha ibada ya misa takatifu,picha na Serengeti Media Centre.

Na Serengeti Media Centre
Ili kuachana na siasa zisizokuwa na tija ,watu wenye ushahidi wa  mgombea urais kwa tiketi ya Chadema Edward Lowassa  kuwa ni fisadi,waweke wazi  ili vyombo vinavyohusika vichukue hatua kwa maslahi ya taifa.  
Paroko wa Kanisa Katoliki Mugumu wilaya ya Serengeti Alois Magabe katika mahubiri ya ibada takatifu ya kwanza nay a pili ,amesema kwa serikali yenye kuheshimu utawala wa sheria,haiwezekani tuhuma za mtu zikatolewa kwenye majukwaa badala ya kukabidhi vyombo vinavyohusika aweze kushughulikiwa.
“Karibu miaka kumi tunasikia fisadi fisadi,mla rushwa,hakuna anayetoka na kuweka wazi tuhuma zake wananchi tuzijue ,tunashuhudia wezi,wenye makosa na tuhuma mbalimbali wanakamatwa na kufikishwa mahakamani,wengine wananchi wanawaua ….kwanini huyu anatajwa majukwaani hafikishwi kwenye vyombo vya sheria,au ni chuki binafsi?,”amehoji.
Padri Magabe amesema siasa kama hizo haziwasaidii wananchi kufikia maamzi sahihi kwa kuwa hazina tija,”mimi si mshabiki wa Chadema wala CCM,lakini nakerwa na siasa za namna hii,nchi hii ina maadili ya viongozi,utawala bora,inakuwaje Takukuru,Usalama wa Taifa,Polisi,wapelelezi na Mahakama wapo,kwanini hafikishwi kwenye vyombo hivyo,maana majukwaa hayashughulikii waharifu,”amebainisha na kuongeza.
“Kwa wakristo katika Zaburi ya 15 inasema,Bwana ni nani atakayekaa katika hema yako,atakayefanya maskani yake katika kilima chako kitakatifu…ni mtu aendaye kwa ukamilifu na kutenda haki,asemaye kweli kwa moyo wake,asiyesingizia kwa ulimi wake,wala hakumtendea mwenziwe mabaya”amesema.
Amesema imefikia hatua hata kama kuna ukweli ama la ,wananchi hawaamini kwa kuwa suala moja linazungumzwa kwa miaka mingi,lakini anayetuhumiwa hafikishwi kwenye vyombo vya dola,maana kama amesababisha  athari kubwa kwa jamii inawezekanaje apate sifa za kugombea,na asikamatwe.
Amevitaka na vyombo vya habari visiishie kuandika na kutangaza kama wanavyosema wanasiasa,bali wafanye uchambuzi na kuanisha tuhuma zake  zake kama zipo  ili wananchi wazijue,kwa kuwa kinachosema ni fisadi,mla rushwa na hakuna anayetoka kukabidhi ushahidi vyombo husika,badala yake ni  kuichafua familia hiyo bila kosa.
Amehoji Lowassa  ana uwezo gani wa kuvishinda vyombo vya dola ,badala yake anasemwa majukwaani na ameshiriki shughuli nyingi za kijamii ,kwa kipindi chote na kushika nafasi mbalimbali ndani ya kamati zao za bunge ,na hao hao ndiyo walimchagua,sasa wananchi watawaminije kwa wanayosema leo.
Kuhusu tuhuma za utajiri anaotajwa nao,amesema Azimio la Arusha lilikuwa na misingi mizuri juu ya viongozi,kwa matajiri walibanwa na kodi,”kazi ya serikali ni kutoza kodi kwenye shughuli zake zinazompa utajiri,kama halipi waseme ili wananchi wamjue mapema ,”alisisitiza.
Akizungumzia sera ya mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi(CCM)John Magufuli  ya kuanzisha  chombo cha kushughulikia wala rushwa na mafisadi, kuwa ni ya Chadema ,hata hivyo amesema kutokana na rekodi yake iwapo atashinda anaweza kusimamia sera hiyo na kuwabana watuhumiwa wote.
Amekemea siasa za matusi na chuki zinazotolewa na viongozi na kuwataka waeleze mikakati yao  ili  wananchi wapime nani amejipanga kuliondoa taifa katika matatizo yaliyopo.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment