Fahari ya Serengeti

Friday, August 21, 2015

UKAWA WASAMBARATIKA-SERENGETI.

 Mgombea Ubunge kwa tiketi ya ACT WAZALENDO jimbo la Serengeti Thomas Burito kulia akitinga ofisi ya afisa uchaguzi jimbo hilo kurudisha fomu.
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM Dk Stephen Kebwe akiwasilisha fomu za kugombea ubunge jimbo hilo kwa Msimamizi wa Uchaguzi wilaya Naomi Nnko.

  Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)Jimbo la Serengeti Dk Stephen Kebwe akiwasilisha fomu zake kwa msimamizi wa Uchaguzi jimbo hilo Naomi Nnko.
 Msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo akiweka sahihi kukiri kupokea fomu za mgombea huyo.
 Dk Kebwe akiagana na Msimamizi wa Uchaguzi.


 Mosena Nyambabe mgombea ubunge kwa tiketi ya Nccr Mageuzi jimbo la Serengeti akiwasilisha fomu kwa msimamizi wa Uchaguzi jimbo hilo Naomi Nnko.
 Anaweka sahihi kukiri kurudisha fomu

 Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Serengeti Naomi Nnko akiongea na Mosena Nyambabe,aliyesimama ni afisa uchaguzi jimbo hilo Prosper Ndiva akipitia fomu za mgombea huyo baada ya kurudisha.
 Mosena Nyambabe akiwa na viongozi wa chama hicho katika ofisi ya Afisa Uchaguzi wilaya.
 Msimamizi wa Uchauguzi jimbo la Serengeti Naomi Nnko akiwa na afisa uchaguzi Prosper Ndiva wakijadiliana na mgombea Ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya Nccr Mageuzi Mosena Nyambabe,hayupo pichani.
 Mosena Nyambabe Mgombea Ubunge jimbo la Serengeti akisalimiana na Msimamizi wa Uchaguzi wilaya Naomi Nnko .
 Mgombea Ubunge jimboa la Serengeti kwa tiketi ya Nccr Mageuzi ambaye pia ni Katibu Mkuu Taifa wa Chama hicho,kushoto Mosena Nyambabe akiwa na viongozi na wanachama wa chama hicho mara baada ya kurudisha fomu ya kugombea Ubunge.
Mgombea Ubunge kupitia Act Wazalendo Thomas Burito kulia akiwa amekaa na viongozi wa chama hicho katika ofisi ya Afisa uchaguzi wilaya ya Serengeti ,muda mfupi baada ya kurusdisha fomu.


UKAWA WASAMBARATIKA-SERENGETI
Na Serengeti Media Centre
Agosti 21,2015
Umoja wa Katiba ya Wananchi(Ukawa)wilayani Serengeti Mkoa wa Mara umesambaratika,na kila chama kinachounda umoja huo kimesimamisha mgombea ubunge ,na udiwani kila kata.
Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika wilaya hiyo vyama vya Nccr Mageuzi na Chama cha Wananchi(CUF)viliunda Umoja wao baada ya kushindwa kuelewa na uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema)waliotaka kuachiwa vijiji na vitongoji vingi,ikiwemo maeneo ambayo vyama hivyo vilikuwa vinaongoza.
Mwenyekiti wa Chadema wilaya Manawa Sang’uda akiongea na Serengeti Media Centre kwa njia ya simu amesema pamoja na kuwa hawana waraka kutoka Makao Makuu ya chama chao kuhusiana na kumteua Mgombea Ubunge jimbo hilo,wameamua kuchukua fomu na kurudisha.
“Makao makuu wameniambia kuwa jimbo hili tumepewa sisi,ingawa hawajatuma waraka wowote kuhusiana na uamzi huo….imetupa wakati mgumu sana maana katika orodha ya majina ya wagombea mkoa wa Mara,yapo majina ya wagombea tisa na jimbo hili halipo”amesema.
Serengeti Media Centre ilipomuuliza taarifa zilizozagaa jimboni humo kuwa Chama cha Nccr Mageuzi kati ya majimbo waliyoongezewa na hilo limo,alikiri kusikia taarifa hizo,”ni kweli nimesikia lakini sasa makao makuu nao wanasema mgombea wetu ndiye anayegombea”amebainisha.
Kuhusu madiwani ,Mwenyekiti amesema kuwa haitawezekana kwa kuwa muda umekwisha na wanaanza kampeini,”ni vigumu kwa sasa,Toolate”amedai Mwenyekiti.
Akiongea na SMC mgombea ubunge kupitia chama cha Nccr Mageuzi ambaye pia ni Katibu Mkuu Taifa wa Chama hicho Mosena Nyambabe,amesema yeye ndiye amepewa jimbo hilo kupitia Ukawa ,ikiwa ni kutekeleza azimio la kikao cha Umoja huo kilichofanyika Zanzibar.
“Miongoni mwa makubalino yalikuwa ni palipo na kiongozi Mkuu wa Kitaifa wa Chama anapewa nafasi ya kugombea,na ndicho killichofanyika hapa….katika majimbo kumi ya mkoa wa Mara ,sisi tumepewa moja hili la Serengeti,nadhani wenzetu wanapaswa kuheshimu makubaliano hayo na wasitake kila kitu wenyewe”anasema.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi(CUF)wilaya hiyo Joseph Rhobi amesema kuwa amejitahidi kuhakikisha vikao vinakaa ili waweze kugawana kata na namna ya kuendesha kampeini kwa umoja wao ili waweze kushinda.
“Vikao viwili tulivyokaa Chadema hawakufika kabisa,tulikutana ofisi ya Nccr mageuzi,wenzetu wakadai hawana nafasi,wana vikao vya uteuzi,wakapanga tukutane jioni ofisi ya Cuf wilaya…..hawakufika wala hawakutoa taarifa,sisi na Nccr Mageuzi tumeunda umoja wetu kama ilivyokuwa uchaguzi wa serikali za mitaa,maana hawataki”amesema kwa masikitiko.
Smc ilipotaka ufafanuzi kutoka kwa Mwenyekiti wa Chadema,amekiri kutohudhuria kwa madai kuwa alikuwa na majukumu,hata hivyo amekiri kupokea waraka kutoka makao makuu ya chama chake kuwataka wakae wagawane kata kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.
Wakati huo huo wagombea wa vyama vya Wananchi (CUF)Emakulata Mniko,Thomas Burito(Act wazalendo)Dk Stephen Kebwe(CCM)Marwa Ryoba(Chadema)na Mosena Nyambabe(Nccr Mageuzi(Nccr Mageuzi,wamerudisha fomu za kuwania Ubunge jimbo hilo.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment