Fahari ya Serengeti

Tuesday, August 18, 2015

MGOMBEA UBUNGE KUPITIA ACT WAZALENDO -SERENGETI ACHUKUA FOMU,

 Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Serengeti Mkoa wa Mara ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Naomi Nnko akipitia nyaraka mbalimbali wakati mgombea ubunge jimbo hilo kupitia ACT-WAZALENDO Thomas Burito anachukua fomu ya kuwania nafasi hiyo.
 Mgombea Ubunge kupitia Act Thomas Burito na uongozi wa chama hicho wilaya wakiwa wamekaa wakimsikiliza afisa uchaguzi wa jimbo hilo Prosper Ndiva aliyesimama akitoa maelekezo ,aliyekaa ni msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo.
 Afisa uchaguzi jimbo la Serengeti Naomi Nnko akimkaribisha rasmi mgombea ubunge jimbo hilo kupitia Act Wazalendo Thomas Burito.
 Msimamizi wa Uchaguzi akitoa mwongozo kwa Thomas Burito mambo muhimu ya kuzingatia ili asipoteze sifa ya kuteuliwa kuwania ubunge jimbo hilo.
 Msimamizi wa uchaguzi akimkabidhi fomu za kutafuta wadhamini Thomas Burito(ACT)wa kwanza kulia ni katibu wa Act wazalendo wilaya Yohana Dise,Mwenyekiti wa wilaya Stephen Masatu
 Msimamizi wa uchaguzi akimpongeza mgombea na kumtakia heri katika mchakato huo akisisitiza kuzingatia masharti yaliyomo ndani ya fomu.


 Burito anasaini kupokea fomu zote.

 Wanaagana
 Wanachama na mashabiki wa CCM jimbo la Serengeti  wakiwasili halmashauri ya wilaya wakimsindikiza mgombea ubunge jimbo hilo Dk Stephen Kebwe.
 Dk Kebwe akiwa na viongozi wa chama wilaya,nje ya lango la kuingia halmashauri wakijadiliana kabla ya kuingia ndani.

 Dk Kebwe akisindikizwa na viongozi na wanachama mbalimbali wa chama hicho kuelekea ofisi ya Msimamizi wa uchaguzi wilaya.
 Msimamzi wa uchaguzi akitoa maelezo kwa mgombea aliyekaa na viongozi na wananchama wa chama hicho.
 wanasikiliza kwa makini maelekezo ya msimamizi wa uchaguzi.
 Msimamizi akitoa ufafanuzi.
 Msimamzi wa uchaguzi jimbo hilo Naomi Nnko akimlabidhi dk Kebwe fomu za kutafutia wadhamini na kanuni za kuzingatia.
 Hata hawa walikuwepo
 Anapokea fomu

 Dk Kebwe akisaini kupokea fomu za kugombea

 Msafara wa kuondoka ukiongozwa kwa pikipiki unaanza kuondoka kuelekea ofisini wakihanikizwa na tarumbeta
 Dk Kebwe akiwa kwenye boda boda


ACT WAZALENDO,CCM WACHUKUA FOMU ZA UBUNGE
Na Serengeti Media Centre.
Agosti 18,2015
 Serengeti:Wagombea Ubunge jimbo la Serengeti Mkoa wa Mara wameaswa kuepuka kufanya kampeini kabla ya wakati ,na wanatakiwa kuzingatia kanuni na maadili ya uchaguzi kama ilivyoelekezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Akikabidhi fomu kwa wagombea Ubunge wa vyama vya ACT-Wazelendo Thomas Burito na Dk Stephen Kebwe (CCM)kwa nyakati tofauti Msimamizi wa Uchaguzi jimbo hilo Naomi Nnko katika ofisi ya Afisa uchaguzi,alisema ili kuepukana na siasa zisizostahili wanatakiwa kusoma vema vitabu vya maadili.
Alisema kila mgombea anatakiwa kutafuta wagombea wenye sifa kama ilivyoelekezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi,na si kufanya kampeini kwa kuwa muda wake haujafika ,na watakao kiuka taratibu hizo watakuwa wamepoteza sifa za kuteuliwa kugombea.
“Zingatieni maelekezo yote  kama yalivyoanishwa kwenye fomu za kugombea ,maana zina makatazo ambayo yanatakiwa kuzingatiwa ,kinyume chake mtawekewa pingamizi na kukosa sifa za kugombea,”alisema.
Akiongea na Serengeti Media Centre mgombea ubunge kupitia Act Wazalendo Burito alisema iwapo atapata ridhaa ya kuchaguliwa atatumia  mfuko wa jimbo kuwalipia bima afya watu wasiokuwa na uwezo ili waweze kuwa wanapata matibabu.
“Wilaya yetu ina utajiri mkubwa wa rasilimali,hazijatumika kutatua matatizo ya wananchi kutokana na kukosekana kwa mwakilishi makini,mimi natarajia kuifanya kazi hiyo ili kutoa tafsri halisi ya jina lenye sifa kubwa duniani lakini wananchi hawana maji safi ya kunywa,watoto wanakaa chini “alisema.
Kwa upande wake Dk Kebwe(CCM)alisema akichaguliwa atatekeleza mambo yaliyoanishwa ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya 2015-2020,na  kutumia juhudi binafsi atahakikisha mtandao wa maji unasambaa kwa asilimia 65 vijijini na asilimia 90 mjini.
“Kwa kushirikiana na wenzangu tunapambana kuhakikisha mji wa Mugumu unakuwa kitovu cha utalii,ili kufikia malengo hayo tutahakikisha barabara ya Lami Makutano ,Mugumu hadi Loliondo inakamilishwa na barabara za mji zilizokwishaanza kutengenezwa kwa kiwango cha lami zinaungwanishwa”alisema.
Kwa upande wa afya alisema watahakikisha wanakamlisha ujenzi wa hospitali ya halmashauri na kuipatia vifaa,”kwa juhudi binafsi tayari marafiki zangu wa Marekani wamekubali kuleta vifaa vyenye thamani zaidi ya  sh 3 bilioni,ambavyo vitatumika wilayani hapa ili kuondoa adha huko vijijini,”alisema.
Wagombea wanne wameishachukua fomu,Emakulata Mniko(CUF)Mosena Nyambabe(Nccr-Mageuzi)Thomas Burito(Act Wazalendo)na Dk Stephen Kebwe(CCM)
Mwisho.



0 comments:

Post a Comment