Fahari ya Serengeti

Monday, August 17, 2015

KATIBU NCCR MAGEUZI TAIFA ACHUKUA FOMU YA UBUNGE-SERENGETI

 Katibu wa chama cha Nccr Mageuzi Taifa Mosena Nyambabe kulia akimkabidhi afisa uchaguzi jimbo la Serengeti Mkoa wa Mara Prosper Ndiva kushoto barua ya uteuzi ndani ya chama kuwania nafasi ya ubunge jimbo hilo,mwanzoni ni mwenyekiti wa chama hicho wilaya Tanu Mwita.
 Nyambabe akimkabidhi nyaraka mbalimbali kabla ya kukabidhiwa fomu ya kutafuta wadhamini kabla ya uteuzi wa kuwania ubunge jimbo hilo.
 Afisa uchaguzi jimbo la Serengeti Ndiva akitoa maelekezo mbalimbali ya tume kwa mgombea aliyeambata na viongozi wa wilaya hiyo.
 Anatoa maelekezo ya kuzingatia

 Nyambabe anapokea fomu ya kuwania ubunge jimbo hilo
 Afisa uchaguzi anapitia fomu huku akitoa maelekezo kuwa wasianze kampeini kabla ya uteuzi
 Anapokea nyaraka



Sasa kazi ya kutafuta wadhamini waliojiandikisha katika daftari la wapiga kura.



KATIBU MKUU NCCR MAGEUZI ACHUKUA FOMU,
Na  Serengeti Media Centre
Agosti 17,2015
Katibu Mkuu Taifa  chama cha Nccr Mageuzi Mosena Nyambabe amechukua fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Serengeti Mkoa wa Mara na kuanika  vipaumbele vyake.
Akiongea na Serengeti Media Centre (SMC) baada ya kukabidhiwa fomu na afisa uchaguz jimbo hilo Prosper Ndiva,Nyambabe amesema mambo ya kuanza nayo ni madai ya walimu,kwa kuwa hayahitaji fedha zaidi ya kufuatilia,uboreshaji wa elimu ,matumizi sawa ya mapato ya wilaya na migogoro ya wakulima na wahifadhi.
Amesema matatizo ya walimu yanajulikana na kinachotakiwa ni ufuatiliaji kwa ngazi husika ili waweze kulipwa stahiki zao na waweze kufanya kazi kwa ufanisi,”nikipata ridhaa nitahakikisha tatizo hilo linakwisha,maana halihitaji fedha…nitashughulikia suala la miundo mbinu ya elimu kama maabara na vifaa ,maana mazingira yalivyo hayatoi nafasi  nzuri kwa walimu kufundishia na watoto kujifunzia”amesema.
Nyambabe amesema ili kutoa elimu nzuri na kuzalisha watu wenye weledi ataelekeza nguvu kuboresha maabara na vifaa vyake kwa shule za sekondari,na shule za msingi atahakikisha wanaboresha miundo mbinu.
Kuhusu mgawanyo sawa wa raslimali za umma zinazopatikana amesema ataondoa kasumba iliyokuwa imejengeka kubagua baadhi ya maeneo kimaendeleo,tabia ambayo amesema haijengi umoja wa wilaya.
“Wilaya yetu inazungukwa na maeneo yaliyohifadhiwa yenye wanyama kama tembo na mengine yana wawekezaji..wananchi walitakiwa kunufaika na raslimali hizo,badala yake wanazidi kuwa maskini maana wanacholima hawavuni,tembo wanakula mazao ,watu wanauawa na wengine kujeruhiwa ,lakini hawalipwi nitayatafutia ufumbuzi,”anasema.
Katibu Mkuu huyo amesema serikali na wadau wa uhifadhi kushindwa kushughulikia matatizo hayo ni chanzo cha wananchi kuona uhifadhi kama balaa badala ya baraka,hivyo atahakikisha kunawekwa utaratibu mzuri wa kupunguza madhara kwa wananchi ili waweze kushiriki uhifadhi wa wanyamapori.
Akizungumzia Ukawa amesema kati ya majimbo kumi mkoani Mara Nccr Mageuzi wamepewa jimbo moja tu la Serengeti kwa kuzingatia tafiti zilizofanywa na wataalam wa Ukawa ,pia makubaliano wa viongozi wa Umoja kuwa walipo viongozi wakuu wa kitaifa wanaachiwa jimbo.
 “Vigezo vyote vimefuatwa na nimeteuliwa kugombea jimbo hili,chama chetu kimekubali kuachia majimbo tisa ya mkoa wa Mara na kusimamisha hili tu….mimi kama katibu mkuu mwenza taifa wa Ukawa nilikubaliana na kuachia majimbo mengine na hivyo,ndani ya chama nimeteuliwa kuwania nafasi hiyo”amesema.
Hata hivyo Emakulata Mniko kutoka Chama cha Wananchi (CUF)kinachounda Ukawa amekuwa mgombea wa  kwanza kuchukua fomu ya kuwania ubunge jimbo hilo.
Afisa Uchaguzi jimbo hilo Ndiva amesema kuwa wanatakiwa kutafuta wadhamini na kurudisha fomu zao agosti 21 kwa ajili ya uteuzi na hawaruhusiwi kuanza kampeini.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment