Fahari ya Serengeti

Friday, August 28, 2015

WANANCHI WANAOTUHUMIWA KUSABABISHA MAUAJI WASUSA MAZISHI,



Wauguzi ,waganga na madaktari wa hospitali Teule ya Nyerere wilaya ya Serengeti walijitahidi sana kuokoa maisha ya Nyantito Robert mkazi wa kijiji cha Bwitengi,ambaye alichomwa mshale kifuani,juhudi zao hazikuzaa matunda,aliaga dunia.
Serengeti Media Centre(SMC)
Agosti 28,2015
Serengeti:Wakazi wa Kijiji cha Bwitengi wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara wanaodaiwa kuvamia mji wa Robert Ntantato na kusababisha kifo,kujeruhi,kubomoa mji na kupora vitu,wamesusa shughuli za  mazishi ya mwanakijiji mwenzao.
Uamzi huo unadaiwa ni mwendelezo wa msimamo  wa vijiji vitano vya Bwitengi,Morotonga,Rwamchanga,Miseke na Parknyigoti waliouweka agosti 26 mwaka huu kupitia mkutano wa Jamii(Ritongo),kuhamisha familia ya Robert Nyantato,aliyewashitaki baada ya kumnyang’anya ng’ombe tano kufuatia kijana wake kukamatwa kwa tuhuma za wizi wa ng’ombe mmoja.
Paulo Boche mkazi wa kijiji cha Burunga alisema ,mazingira hayo yaliwalazimu majilani  kusaidia shughuli za mazishi baada ya wakazi wa kijiji hicho kususia kwa madai kuwa ametengwa na jamii hiyo.
“Sisi kijiji jilani cha Burunga na ndugu zake ndiyo tumeshiriki shughuli za mazishi ya Nyantato Robert ambaye anadaiwa kuchomwa mshale agosti 26 nyumbani  kwao mwaka huu na kufia hospitali,kitendo hiki kwa kweli kimetusikitisha sana”alisema.
Alisema hakuna matanga yatakayofanyika,”kwa mila na desturi mtu akiuawa katika mazingira kama haya hakuna matanga….na huzikwa nje ya mji kwa kuwa huchukuliwa ni mkosi katika familia”alisema.
Rpc,
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mara Philip Karangi akiongea na  Serengeti Media Centre(SMC) kwa njia ya simu ,alisema watu tisa wameishakamatwa kuhusiana na tukio hilo ambao ni wakazi wa kijiji hicho.
“Tunaendelea na msako na wote wanaotuhumiwa watakamatwa ,wananchi watambue kuwa kujichukulia sheria mkononi ni kosa kubwa….tunahimiza utawala wa sheria,hatutamuacha hata mmoja anayevunja sheria,”alisema.

habari kutoka vijiji hivyo zinadaiwa kuwa watu wengi wamekimbilia porini wakikimbia kukamatwa kutokana na tuhuma za kuua,kujeruhi,kubomoa nyumba na kupora mali za Robert Nyantato.
 
Wanaharakati,
Mwenyekiti Mtendaji wa shirika la Wasaidizi wa Kisheria na Haki za Binadamu Samwel Mewama alisema,serikali kuruhusu vikao visivyokuwa vya kisheria kutoa uamzi unaokinzana na sheria za nchi ndiyo matokeo yake.
“Jadi iko juu ya serikali hapa,wanaweza kukaa na kuamua kumhamisha mtu,kupora mali zake,kuua,kuchoma mji ,lakini serikali imekuwa kimya sana na matokeo yake yanasababisha taswira mbaya ya wilaya na jamii ya Waikoma,”alisema.
Ilivyotokea.
Agosti 11 mwaka huu eneo la mnada wa Mugumu  Sanja Robet(27)ambaye ni kijana wa Robert Nyantato alikamatwa na ng’ombe mmoja anayedaiwa kuwa wa wizi,na kufikishwa polisi.
Pamoja na kufikishwa polisi kwa hatua za kisheria ,wananchi walivamia makazi ya Nyantato ambaye ni baba yake na kuchukua ng’ombe tano kwa kosa alilotenda kijana wake ambaye ana mji wake.
Hata hivyo alifikisha malalamiko polisi na ofisi ya Mkuu wa wilaya ,wananchi wakaamriwa warudishe ng’ombe hizo ,na agosti 26 mwaka huu waliahidi kurudisha.
Katika kikao cha wananchi hao kwa mwanvuli wa jadi(ritongo)agenda ya kurudisha ng’ombe ilikataliwa na kuamua kumtenga,kumhamisha hapo kijijini,katika utekelezaji huo walimchoma mshale kifuani Nyantato Robert na kusababisha kifo.
Pia walimjeruhi Robert Nyantato ,kubomoa nyumba na kupora vitu mbalimbali ikiwemo mifugo.
Matukio Mengine kwa jamii hiyo,
Mwanzoni mwa mwaka huu kupitia vikao vya ritongo watu watano katika kata ya Ikoma waliuawa ,wengine makazi yao kuteketezwa,kuhamishwa kwa kutuhumiwa kujihusisha na matendo ya uchawi.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment