Fahari ya Serengeti

Friday, August 28, 2015

WATEKA GARI,PIKIPIKI,KUPORA NA KUJERUH



eddted.jpg
Na SERENGETI MEDIA CENTRE(SMC)
Agosti 28,2015


 Mkazi wa kijiji cha Nyichoka wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara,Mahiri Nchagwa(30)akiwa amelazwa katika hospitali Teule ya Nyerere kufuatia kushambuliwa na watu wanaodhaniwa majambazi,picha na Serengeti Media Centre.

Watu wawili wamejeruhiwa mmoja akiwa na hali mbaya baada ya kutekwa kupigwa,kuporwa fedha na watu wanaodhaniwa  kuwa majambazi walioteka gari na pikipiki katika kijiji cha Burunga wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mara Philip Karangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo,agosti 27 majira ya kati ya saa 2na 3 usiku mwaka huu,watu wasiojulikana walitega magogo na kuteka pikipiki ,Hiace ,kupora na kujeruhi.
Mmoja wa majeruhi Mahiri Nchagwa(30) ambaye amelazwa katika hospitali Teule ya Nyerere wilayani hapa kutokana na kujeruhiwa vibaya,alisema alitekwa na watu watano waliokuwa na mapanga,na marungu na kumkata kata ,kumpora sh 300,000 ,simu na ufunguo wa pikipiki.
“Nilikuwa natokea mjini kuuza maziwa ,nilipofika eneo hilo niliona matawi ya miti,nikadhani kuna gari limeharibika,nikasogea taratibu nikakuta magogo makubwa yamewekwa barabarani….kusimama ghafla nikavamiwa na watu watano”alisema na kuongeza.
“Mbele yangu kulikuwa na watu wawili waliovalia kofia za kufunika uso,makoti marefu wana mapanga na rungu,nyuma walikuwepo watatu,wakaanza kunishambulia kwa kunikata kata kwa panga,na kunipiga kwa rungu,wakachukua fedha za mauzo,funguo na simu “alisema kwa kugugumia.
Majeruhi huyo alisema wakati wanamshambulia lilitokea gari aina ya Hiace lililokuwa linatokea Bunda ,wakamuacha na kwenda kuwashambulia waliokuwa ndani ya gari,akafanikiwa kukimbia huku akipiga yowe na kusaidiwa na mtu mmoja ,aliyemfikisha hospitali kwa matibabu.
Hata hivyo hakuweza kuwatambua watu hao kwa kuwa kulikuwa ni giza na walikuwa wameficha nyuso zao,Kamanda wa polisi Mkoa wa Mara hakuweza kutaja namba za gari na pikipiki,na alikiri kuwa hakuna mtu anashikiliwa kutokana na tukio hilo,na uchunguzi unaendelea.
Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo Emiliana Donald alisema majeruhi huyo anaendelea na matibabu,ingawa amejeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili,na kuwa majeruhi mwingine Samsoni Jeremia(24)mkazi wa Bunda ameruhusiwa kutoka baada ya kupata matibabu.
Matukio ya watu kutega magogo na kuteka magari ya abiria yanayotoka Bunda jioni yameanza kujitokeza tena,ambapo mwaka 2011/12,uharifu huo ulishamiri .
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment