Fahari ya Serengeti

Wednesday, August 26, 2015

WANANCHI SERENGETI WADAIWA KUUA,KUJERUHI,KUBOMOA NYUMBA NA KUPORA VITU

Familia ya Roberi Nyantato mkazi wa kitongoji cha Mtakuja kijiji cha Bwitengi wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara wakisomba vitu kutoka maeneo tofauti,baada ya wakazi wa vijiji vya Morotonga,Bwitengi,Rwamchanga,Miseke na Park nyigoti kuvamia mji wake,na kumchoma mshale kijana wake Nyantato Robert na kusababisha kifo,kujeruhi mzee,kubomoa mji na kupora vitu,baada ya kuagizwa wamlipe ng'ombe wake watano waliochukua wakituhumu kijana wake kuiba ng'ombe mmoja,hata hivyo mtuhumiwa ameishafikishwa mahakamani kwa kosa la kudaiwa kuiba ng'ombe.
Utafutaji wa vifaa unaendelea kufuatia maamzi yasiyozingatia haki za binadamu yaliyofanywa na kundi la wananchi kwa kivuli cha Ritongo.
Nyumba hiyo ilibomolewa madirisha na milango na kuanza kutoa vitu kwa madai ya kumtenga na kumhamisha kwa kuwa aliwashitaki kwa kupora ng'ombe tano na kuuza kwa tuhuma za kijana wake ambaye anajitegemea .
Baamda lililokuwa na nguruwe na mifugo mingine limebomolewa na wananchi hao.

Hapo wanaendelea kukusanya vitu na mifugo ,hata hivyo wanadai baadhi ya vitu na mifugo vimepotea.

Baadhi ya ndugu wakisaidia kusomba vitu
Polisi walifika kushuhudia unyama huo unaofanywa kwa mwanvuli wa Ritongo
Hali ilikuwa hiv.o
Robert akisaidia na mjukuu baada ya kupigwa na kuumizwa wakati anasaidia kijana wake ,hata hivyo aliaga dunia kutokana na shambulio la mshale ulioharibu mishipa ya moyo.

Watoto na wajukuu wakiwa hawajui nini la kufanya
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Bwitengi,Bwigeki alishuhudia unyama huo.
Baadhi ya vifaa vilivyopatikana.
Majeruhi anapelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu
Ndugu wakiwa hospitali Teule ya Nyerere wakisubiri majibu ya madaktari kuhusiana na ndugu yao aliyechomwa mshale,hata hivyo aliaga dunia
Robert akiwa hospitali akisburi mkupata huduma
Picha ya Xray ikionyesha mshale ulivyokita sehemu ya moyo.

0 comments:

Post a Comment