Fahari ya Serengeti

Monday, September 7, 2015

KUHAMISHWA KWA MWALIMU KWAZUA TAHARUKI KWA WAZAZI

Na Serengeti Media Centre
Wakazi wa kijiji cha Mesaga kata ya Kenyamonta wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara,wamemtaka Mkurugenzi Mtendaji kutohamisha walimu kwa shinikizo la watu,kwa kuwa inachangia kushuka kwa taaluma.
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Chacha Getumbe amesema hayo katika mkutano wa hadhara wa kijiji ulioitishwa kupinga uhamisho wa Mwalimu  wa shule hiyo Jimmy Ambrose kwenda shule ya Msingi Kisaka,kuwa unatokana na kutoelewana kwa mwalimu huyo na  Padri wa Kanisa Katoliki Iramba Johnson Kitunzi.
Amesema  shule hiyo yenye wanafunzi 527 ina hitaji walimu 12 ,lakini ina walimu 6 ,na kuwa mwalimu huyo amehamishiwa kijijini hapo mwaka jana ili amuuguze mama yake ambaye ni kipofu ,kutolewa kwake watabaki  walimu watano na watoto wao wataathirika kitaaluma.
Afisa elimu wilaya William Mabanga amekiri kuwepo kwa mgogoro kati ya Padri na Mwalimu kwa masuala ya Kwaya,na kuwa ameishapokea  malalamiko ya wananchi na mwalimu mwenyewe,na kudai wamesitisha uhamisho huo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Victor Rutonesha amesema suala hilo litaangaliwa upya,na kudai kuwa taratibu za uhamisho uzingatia sheria za utumishi wala si shinikizo.
Akiongea na Serengeti Media Centrea kwa njia ya Simu Padri Kitunzi amekiri kuwepo mgogoro kati yake na Mwalimu huyo,lakini amekana kuhusika na uhamisho wake kwa kuwa yeye hausiani na masuala ya serikali.

Viongozi wa kijiji cha Mesaga kata ya Kenyamonta wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara wakiwa kwenye mkutano wa hadhara kujadili hoja ya kupinga kuhamishwa kwa mwalimu wa shule ya Msingi Mesaga Jimmy Ambrose kwa shinikizo la Padri Johnson Kitunzi wa kanisa katoliki Mugumu baada ya kutoelewana.
Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara kupinga uhamisho huo ambao wanadai una madhara kitaaluma kwa watoto wao.

Baadhi walishauri waandamane kwenda ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupinga uhamisho huo uliofanywa kwa maslahi ya mtu na kuathiri taaluma kwa watoto wao.
Wnatoa msimamo wao.

0 comments:

Post a Comment