Fahari ya Serengeti

Wednesday, September 9, 2015

MAHAFALI YA 15 CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA -KISARE WILAYA YA SERENGETI

Na Serengeti Media Centre
Ili kukabiliwa na upungufu wa wataalam katika sekta ya Afya hapa nchini,Chuo  cha Sayansi za Afya   Kisare wilayani Serengeti Mkoa wa Mara kinatarajia kuanzisha kozi mbalimbali za utabibu.
Mkuu wa chuo hicho Joachim Urassa akitoa taarifa katika mahafali ya 15 ya chuo hicho yaliyofanyika mwishoni mwa wiki ,alisema wanatarajia kuanzisha kada za afya ,ikiwemo Stashahada ya Utabibu,Maabara,Afya ya Mazingira na Famasia.
“Leo wamehitimu wataalam 120 ngazi ya vyeti na Stashahada katika fani za Ukunga na Uuguzi,na wote wanakwenda kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali….lengo ni kuhakikisha wanasaidia jamii kutambua na kushughulikia matatizo yao,na tunayo matarajio ya kuongeza fani nyingine ili kupunguza tatizo la upungufu wa wataalam,”alisema.
Hata hivyo alikiri kuwepo kwa changamoto za jamii na  taasisi mbalimbali zilizopo wilayani hapo kutokujitokeza kuchangia uboreshaji wa chuo hicho,ili kukamilisha bwalo la chakula na jiko na bweni kwa ajili ya wavulana ambao wanaishi nyumba ya kupanga nje ya chuo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho,Mchungaji Abunel Mathube aliwataka wahitimu kutumia vema taaluma yao kuhudumia wananchi,”zingatieni maadili ya kazi,mmefundishwa katika chuo cha kidini,tunategemea mkawe mfano maana mnacheza na maisha ya watu,epukeni rushwa”alisisitiza.
Mapema Mkurugenzi wa hospitali Teule ya Nyerere na Chuo hicho  Dk Musuto Chirangi alisema mafanikio ya kazi ya uuguzi si visingizio bali kuwajibika kwa kuzingatia maadili kama walivyofundishwa,itakuwa imesaidia kutimiza malengo ya mafunzo hayo na kupambana na adui maradhi katika jamii.
Chuo hicho kilichoko chini ya kanisa la Menonite kilianza mafunzo 1998 na kilipata usajili wa muda baraza la Elimu ya Ufundi(NACTE) mwaka 2004,kilipata usajili wa kudumu 2009 na kinaendesha mafunzo ya uuguzi na Ukunga ngazi ya cheti na stashahada.



 Maandamano ya wanachuo kuelekea ukumbi ulioandaliwa
 Wanachuo wanaelekea ukumbini
 Maandamano yanaendelea


 Viongozi wa hospitali,wilaya na chuo wakiwa meza kuu.
 Wanachuo wakiwa wanafuatilia matukio mbalimbali.

 Wanakumbuka kiapo




0 comments:

Post a Comment