Fahari ya Serengeti

Thursday, July 27, 2017

TAKUKURU YAMPANDISHA KIZIMBANI MKURUGENZI WA MUWASA KWA KUGHUSHI NYARAKA

SERENGETI MEDIA CENTRE.

Mara .Mkurugenzi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma  Hawaju Said Gantala (42)amefikishwa katika mahakama ya wilaya Musoma kwa Makosa 15 ya kughushi nyaraka na kujipatia sh 63,400,000 kinyume cha sheria.
Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo  Karimu Mushi ,wakili wa Takukuru Mkoa wa Mara Moses Malewo katika kesi ya Jinai namba 176/2017 aliliambia mahakama hiyo Kuwa Mshitakiwa anakabiliwa na Makosa hayo ya kughushi kujipatia fedha kwanjia  ya udanganyifu  na kuwasilisha nyaraka za kupotosha katika benki zaCrdb na NBC matawi ya Musoma.
Alisema kwa kosa la kwanza hadi la tano Mshitakiwa anakabiliwa na Makosa yakughushi nyaraka za kuingiziwa mshahara (salary slip) za Septemba hadi desemba 2014 ,kughushi nyaraka za kuingiziwa mshahara wa juni,Julai na Agosti 2016 kwa kuonyesha kwamba ni nyaraka halali kutoka MUWASA huku akifahamu Kuwa si kweli.
Alibainisha kuwa katika kosa la sita Gantala ili hali akijua kuwa si kweli aliwasilisha nyaraka za kuingiziwa fedha benki ya Crdb Tawi la Musoma ambazo zilikuwa zikionyesha kuwa katika mwezi septemba na desemba 2014 mshahara wake ulikuwa sh 2,767,549 na kujipatia mkopo wa sh 30 mil kinyume cha sheria.
Malewo aliiambia mahakama kuwa kosa la saba mshitakiwa  katika kipindi cha juni,julai na agosti 2016 alijipatia  mkopo wa sh 34,400,000 kutoka Benki ya Nbc Tawi la Musoma kwa kutumia nyaraka za kuingiziwa mshahara(salary slip) za uongo zikionyesha kwamba mshahara wake ni sh 2,636,179.82 kinyume cha sheria.
Kwa kosa la 8 hadi 13 Gantala akijua ni kosa aliwasilisha nyaraka zauongo za  kuingiziwa mshahara wa mtumishi katika benki ya Crdb na Nbc Matawi ya Musoma akidanganya kuwa ni halali kutoka Muwasa na kujipatia jumla ya  sh 63,400,000 toka benki hizo.
Kwa kosa la 14 Wakili huyo wa Takukuru alisema Gantala alimlaghai Mkuu wa Idara ya Utawala MUWASA Brian D.Moshi kuweka saini hati za kuingiziwa mshahara wa Mtumishi (Salary Slip)kwa miezi ya juni,julai na agosti mwaka 2016 ili zionekane ni hati toka Muwasa.
Alifafanua kuwa alifanya hivyo wakati akijua kuwa si nyaraka halali na zililenga kuzipotosha taasisi hizo za fedha kinyume cha sheria.
Katika shitaka la 15 mshitakiwa alimlaghai Issaya Maswi Nyaibo mkuu wa idara ya fedha MUWASA na kutia saini hati za kuingizwa mshahara wa mtumishi (Salary Slip)za kughushi kwa miezi ya septemba,oktoba na novemba 2014 ili zionekane ni hati halali toka Muwasa wakati akijua ni makosa.
Mshitakiwa amekana mashitaka hayo na yuko nje kwa dhamana ya wadhamini wawili kila mmoja kwa kuwa na hati ya mali isiyohamishika yenye thamani kama kiasi hicho na kesi hiyo itatajwa agosti 22 mwaka huu.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment