Fahari ya Serengeti

Saturday, July 15, 2017

KAMPUNI YA GRUMETI RESERVES LTD YAILIPA IKONA WMA ZAIDI YA SH 1.3 BIL

Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Grumeti Reserves Ltd Ami Seki kulia akimkabidhi Mwenyekiti wa IIkona Wma Elias Nchama kushoto Hundi ya zaidi ya sh 1.3 bil ikiwa ni malipo ya deni za miaka mitatu walilokuwa wanadaiwa na Jumuiya hiyo ya Uhifadhi,ikiwa ni gharama za pango,ushuru wa Vitanda,Upigaji Picha na uwindaji wa kitalii.
Katibu wa Ikona Wma Yusuph Manyanda kulia akisaini makubaliano ya hiyari kati ya Jumuiya hiyo na Kampuni ya Grumeti Reserves Ltd ambayo yanawapa wajibu pande zote za kuheshimu taratibu za uwekezaji na uhifadhi,kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Elias Nchama.
Mwenyekiti wa Ikona Wma Elias Nchama akisaini Makubaliano ya hiari ,kushoto ni Katibu wa Jumuiya hiyo Yusuph Manyanda.
Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Grumeti Reserves Ltd Ami Seki akisaini makubaliano ya hiari kati yao na Ikona ,kulia kwake ni Msaidizi wake David Mwakipesele.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti Simioni Warioba kushoto na Afisa wanyamapori wilaya hiyo John Lendoyan wakisaini makubaliano ya hiari kati ya Grumeti Reserves na Ikona Wma.
Wakili Maganiko Msabi ambaye ni Mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti akitoa maelekezo kabla ya kusaini makubaliano ya hiayo ya kampuni ya Grumeti Reserves na Ikona Wma.
Katibu wa Ikona Wma Yusuph Manyanda akitoa ufafanuzi wa pesa zinazotakiwa kulipwa na Grumeti Reserves kabla ya kusainiana makubaliano ya hiari.
Wanajadiliana
Malipo Malipo Malipo.
Wanafuatilia
Wajumbe wa Bodi ya Ikona na wajumbe wa baraza la Jumuiya hiyo wakifuatilia



Wanasheria hawakucheza mbali kuhakikisha saini zinawekwa mahali husika


0 comments:

Post a Comment