Fahari ya Serengeti

Wednesday, July 19, 2017

LUMUYE LEOPARD CO.LTD KUJENGA KIWANDA CHA KUCHAKATA MAFUTA YA ALIZETI

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Lumuye Leopard Co.Ltd Juma Mugiye Chacha kulia akiwa anateta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk Charles Mlingwa muda mfupi baada ya kutembelea eneo la ujenzi wa kiwanda hicho katika eneo la Tambisa mtaa wa MCU Mugumu wilayani Serengeti.
 Mkuu wa Mkoa wa Mara DkCharles Mlingwa akiangalia shamba la alizeti la Kampuni ya Lumuye Leopard.Co.Ltd
 Kaimu meneja wa Tanesco wilaya ya Serengeti Peter Mtete akitoa maelezo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ,lini Tanesco watafikisha umeme katika eneo hilo linalotarajiwa kujengwa kiwanda,hata hivyo amesema kuwa zinatakiwa zaidi ya sh 20 mil,na shirika halina bajeti hiyo hivyo mwekezaji agharamie gharama hizo.
 Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurdin Babu akielezea mikakati ya wilaya kutekeleza sera ya uwekezaji.
 Afisa Mtendaji wa Kata ya Mugumu Bhoke Ruhinda akisoma taarifa ya kampuni ya Lumuye ambayo inatarajia kujenga kiwanda ambacho kitatoa ajira 400 za kudumu na 300 vibarua ,na uzalishaji wake utakuwa ni lita 30750 za mafuta kwa siku
 Rc akiongea na wananchi wa eneo la Tambisa kuchangamkia fursa hiyo ya uwekezaji
 Anasisitiza jambo
 Mkurugenzi wa Lumuye kushoto akifuatilia maelezo ya Mkuu wa Mkoa wakati anaongea na wananchi kuhusiana na uwekezaji anaotarajia kuuweka.
 Wanateta jambo


0 comments:

Post a Comment