Fahari ya Serengeti

Friday, March 10, 2017

UZINDUZI WA MAZOEZI ILI KUZUIA MAGONJWA YASIYO YA KUAMBUKIZWA SERENGETI KESHO



Uzinduzi wa mazoezi ili kuzuia magonjwa yasiyo ya kuambukiza wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara kufanyika  machi 11 mwaka huu .Mpango huo  ambao ni agizo la Makamu wa Rais Samia  Suluhu ambapo kila   jumamosi ya pili ya mwezi ni siku ya mazoezi ya viungo ili kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukizwa,unaratibiwa na ofisi ya mkuu wa wilaya.



Taarifa ya Katibu Tawala Wilaya Cosmas Qamara kwa vyombo vya habari inabainisha kuwa mazoezi yataanzia ofisi ya Mkuu wa wilaya na kuishi Uwanja wa michezo wa Sokoine ambapo mazoezi mbalimbali ya viungo yatafanyika.

Kwa mjibu wa taarifa hiyo inabainisha kila taasisi inatakiwa kushiriki kikamilifu mazoezi hayo na kuratibu ushiriki wa watumishi wake baada ya mazoezi kukamilika.

Kwa upande wa vijijini amewaagiza viongozi  ikiwa ni pamoja na watendaji  waratibu elimu kata kutoa taarifa katika ofisi yake machi 12 mwaka huu kuhusiana na ushiriki wa jamii .

Hata hivyo baadhi ya wakazi wa mji wa Mugumu wamesema uzinduzi wa mazoezi hayo utasaidia viongozi kuchukua hatua dhidi ya watu waliovamia maeneo ya wazi ambayo yalikuwa wakisaidia vijana kufanya mazoezi mbalimbali ya viungo.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment