Fahari ya Serengeti

Saturday, March 18, 2017

TANESCO WAAHIDI KUSAMBAZA UMEME MAENEO YOTE YA ROBANDA

Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco)wilaya ya Serengeti Mhandisi Magoti Mtani akitoa maelezo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk Charles Mlingwa kushoto jinsi walivyosambaza umeme katika kijiji cha Robanda kwa kupitia chini(Underground)na kuahidi kuwa ya kipaumbele kama Taasisi na wananchi yatapata umeme kwa haraka ili kuharakisha huduma na uzalishaji mali.
Meneja wa Tanesco Mhandisi Magoti Mtani kulia akiwaonyesha mfumo uliotumika kushusha umeme toka juu na hatimaye kushusha chini na kupeleka kijijini ,kushoto mkuu wa Mkoa wa Mara Dk Mlingwa na viongozi wengine wakifuatilia maelezo kwa kuangalia juu ya nguzo.
Ufafanuzi wa mtandao huo unaendelea.
Maelezo ya kitaalam yanatolewa.


Mhandisi Magoti kulia akimwongoza mkuu wa Mkoa wa Mara dk Mlingwa wa pili toka kushoto kuelekea eneo la mradi,wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa halmashauri Juma Porini na katikati ni Dc Nurdin Babu.
Rc dk Mlingwa akiwasili katika kijiji cha Robanda kwa ajili ya kukagua miradi,na mkutano wa hadhara wa kijiji ambapo baadhi ya malalamiko ni suala la Single Entry,mapato ya Wma kutowanufaisha wananchi,Tembo kula mazao na mifugo kuingizwa maeneo ya kambi za kitalii.
Anasikiliza kero.

Hatimaye waliagana katika ofisi ya mkuu wa wilaya.

0 comments:

Post a Comment