Fahari ya Serengeti

Wednesday, January 4, 2017

NDEGE YAANGUKA NA KUTEKETEA KWA MOTO




Serengeti Media Centre
Ndege iliyokuwa imebeba watalii watano raia wa Marekani imeanguka na kujeruhi Marubani wawili wa baada ya  kupata hitilafu na kuanguka kisha kutketea kwa moto  wakati inapaa katika uwanja wa Sasakwa wilayani SerengetI Mkoa wa Mara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Ramadhani Ng’hazi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo januari 2 mwaka huu katika Uwanja mdogo wa ndege wa Sasakwa ulioko chini ya Kampuni ya Grumeti Reserves,baada ndege aina ya CESNA F.406 Mali ya Air Excell iliyokuwa ikiongozwa na marubani Mohammed Selemani akisaidiwa na Fahd Salehe kupata  hitilafu na kuanguka na kuteketea kwa moto.
Alisema  ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 12 siku ya tukio  ilikuwa na abiria watano ambao ni Greg Martin Perelman(60)Susan Perelman(52) Sara Melissa Perelman (23) Danielle Jaffe Perelman(21)Emma Stephanie Perelman(19)ambao ni  familia moja toka nchini Marekani ambao walinusurika .
Alisema baada ya ndege kupata hitilafu na kuanguka  Perelman (baba wa familia hiyo) alifanikiwa kuokoa familia yake yote na marubani wawili raia wa Tanzania ambao walishindwa kutoka kutokana na majeraha waliyopata  wasitekee kwa moto baada ya ndege kulipuka.
“Binafsi namwita shujaa kwa kuwa baada ya kutokea hitilafu wakati wanaanza kupaa marubani walijaribu kutua na kushindikana,na kuanza kuviringika,alichofanya akarusha watoto wake nje kupitia dirishani,kisha mke wake,na baada ya kugundua marubani hawatoki na ndege inaanza kuwaka moto aliingia na kuwatoa ingawa walikuwa wamejeruhiwa,”alisema Kamanda.
Alisema ndege imetekea yote na wachunguzi wa ajali toka Mamlaka ya TCAA wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
Kwa mjibu wa Taarifa ya maandishi ya  Mkurugenzi Mtendaji wa Singita Grumeti Graham Ledger,kuwa wageni watano hawakupata majeraha ,lakini marubani wawili waliopata majeraha walisafirishwa kwenda Nairobi nchini Kenya kwa ndege ya madaktari wa amref (MEDIVAC servive)kwa ajili ya matibabu.
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment