Fahari ya Serengeti

Sunday, January 21, 2018

WAZIRI MKUU AMALIZA ZIARA YA SIKU 7 MARA NA KUACHA MAAGIZO MAZITO

 Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa amehitimisha ziara ya siku saba Mkoani Mara na kuacha maagizo mazito kwa viongozi ikiwemo kusimamishwa kwa Mkurugenzi wa Musawa Saidi Gantala na kuitaka Takukuru kuendelea na uchunguzi wa miradi yote ya Maji baada ya kubainika kutafunwa kwa fedha za miradi hiyo.

Amemwagiza Naibu Waziri Tamisemi na Katibu Mkuu wizara ya Maji na Umwagiliaji kubaki mkoani humo wakifuatilia kwa kina taarifa za Miradi ya Maji kwa kukutana na wahandisi wote wa Maji mkoa huo na kumpa taarifa hivi karibuni.

Amewaagiza viongozi na watendaji kutatua kero za wananchi na wasikae ofisini kwa kuwa kupokelewa kwa mabango kila alikokwenda ni ishara mbaya kiutendaji.

 Viongozi mbalimbali wakifuatilia maelekezo ya Waziri Mkuu katika Ukumbi wa Uwekezaji Musoma




0 comments:

Post a Comment