Fahari ya Serengeti

Sunday, January 14, 2018

SIKU CHACHE BAADA YA MFUNGWA KUKAMATWA KWA UJANGILI WAGENI WASIOJULIKANA KUTIMULIWA ROBANDA

 Wakazi wa kijiji cha Robanda wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara wametoa siku mbili kwa wageni wote wasiojulikana kijijini hapo kuondoka kabla ya kuanzishwa msako mkali,uamzi huo umefikiwa kwenye kikao cha jamii(ritongo)ambapo wamelaani mauaji ya tembo yaliyofanywa na majangili wakishirikiana na mfungwa mkazi wa Kibiti.
Pia wamepiga marufuku watuhumiwa wa ujangili Hamisi Gamaho na Nyamincha kurudi kijijini hapo,pia ndugu zao wameonyeshwa njia ya kutokea kwa kuwa wamekuwa sehemu ya ujangili huo kwa kutokusema ama kukemea vitendo vya ujangili na kuingiza silaha kijijini.
 Kwa pamoja wanasisitiza watuhumiwa wakiachiwa wakikanyaga kijijini watachukua maamzi magumu.
 Mama yake na Hamisi Gamaho mmoja wa watuhumiwa wa ujangili akiwa amewekwa kiti moto na wananchi ambapo wamemtaka kuwapisha kijijini hapo warudi Nyichoka kwa kuwa vitendo vya kijana wake vimedhalilisha jamii nzima ya Robanda.

 Msisitizo ulitolewa


0 comments:

Post a Comment