Fahari ya Serengeti

Monday, January 8, 2018

MFUNGWA ANASWA KWA UJANGILI WA TEMBO SERENGETI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Jafari Mohamed akiangalia moja ya bunduki zilizokamatwa na jeshi hilo kwa kushirikiana na askari wa hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambazo zilikuwa zikitumiwa na majangili walioongozwa na Mfungwa Khamisi  Mussa Bweha kutoa Kibiti Rufiji ambaye alifungwa miaka mitatu mwaka jana kwa kosa la kukamatwa na silaha kinyume cha sheria Mwanza ,Hata hivyo amekamatwa kwa tuhuma za kuua tembo wawili katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti akishirikiana na wenzake watatu wakazi wa wilaya ya Serengeti.
Katika tukio hilo Polisi walifanikiwa kupata bunduki mbili Riffle 458 risasi zake tano katika kijiji cha Robanda na bunduki AK-47 na risasi zake 130 iliyokuwa imefukiwa ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
 wanaangalia vitu vilivyokamatwa


 Mzigo wa risasi ulionaswa










1 comment: