Fahari ya Serengeti

Friday, September 16, 2016

SERENGETI YAFUNGUA KITABU KUCHANGIA WAATHIRIKA KAGERA


Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara imefungua kitabu  cha michango ili kusaidia wakazi wa Mkoa wa Kagera walioathirika na tetemeko la ardhi lililosababisha vifo vya watu 17 ,zaidi ya 200 kujeruhiwa na nyumba na mali kuharibiwa.
Mkuu wa wilaya hiyo Nurdin Babu akiongea na Serengeti Media Centre Afrika Ofisini mwake amesema pamoja na jitihada zinazofanywa na serikali kupitia kwa Waziri Mkuu,nao wameamua kuweka utaratibu wa kuchangia michango mbalimbali kutoka kwa watu watakaoguswa ikiwa ni fedha na vitu ili viweze kuwasaidia wananchi walioathirika.
Amesema kila mwananchi anatakiwa kuguswa na tatizo hilo kwa kuwa limeacha madhara makubwa kwa wananchi wa mkoa huo,njia hiyo ndiyo inayoonyesha uzalendo wa kweli.
Mwisho.


0 comments:

Post a Comment