Fahari ya Serengeti

Monday, September 12, 2016

RC AWATAKA WATAALAM KUWATAFUTIA MASOKO WAKULIMA

 Mkuu wa Mkoa wa MaraDk Charles Mlingwa akiongea na wataalam wa wilaya ya Serengeti.


MSIHAMASISHE KILIMO BILA KUWATAFUTIA MASOMO WAKULIMA.
Serengeti Media Centre.
.Watendaji wa serikali mkoa wa Mara wameombwa kuacha tabia za kuhamasisha wananchi kulima mazao  bila kuwatafutia masoko.
Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk Charles Mlindwa akiwa ziarani wilaya ya Serengeti alisema viongozi wanatakiwa kuwa wabunifu wa kuwatafutia masoko wakulima ili kusaidia kuinua uchumi wao.
Alisema ili kuondokana na dhana hiyo ambayo imechangia wakulima kukata tamaa ,kwa kutambua udhaifu wa watendaji wengi ofisi yake inaandaa program maalum ya uzalishaji ambayo utasaidia upatikanaji wa masoko ya mazao mbalimbali yanayozalishwa mkoani humo.
“Mkoa unazungukwa na wawekezaji wa sekta mbalimbali ambao wanakosa huduma bora za mali zinazozalishwa hapa  na kufuata maeneo mengine hadi nje ya nchi,ni wajibu wa watendaji wa halmashauri kuwa na program maalum nini wanahitaji na kuwasaidia wakulima kuzalisha kwa ubora unaotakiwa,hiyo ndiyo njia ya kuonyesha tija kwa kila mtendaji,”alisema.
Alisema watendaji wengi wanakaa sehemu muda mrefu lakini tija yao haionekani,”watoto wanaposhindwa mwalimu hulaumiwa kwa kuwa ufanisi wake huonekana mdogo,sasa kuna tija gani kwa mtaalam  kupokea fedha wakati hatatui matatizo ya wananchi,huwezi kuhimiza wananchi walime wakati huna  suluhisho la soko harafu ukajivuna,lazima uje na mipango,”alisema.
Kwa upande wa mifugo alisema mkoa huo umekuwa lango la kupitisha na kupeleka nchi jilani ,”mifugo ni zao lazima  wataalam wasaidia wafugaji kufanya mabadiliko kwa kuacha kuhesabu utajiri wao kwa wingi wa mifugo bali watumie uzito na ubora wa mfugo kwa kuwa thamani yake itakuwa juu,”alisema na kuongeza,
“Miongoni mwa mapinduzi makubwa tunatarajia kufanya ni kujenga kiwanda cha nyama mkoani hapa ,hii itatusaidia kuongeza ubora wa mifugo na pia watu watafuga mifugo michache iliyoboreshwa na hapo itakuwa imesaidia kupunguza migogoro ya maeneo ya malisho na sekta nyingine,”alisema.
Diwani wa Kata ya Nyansurura Francis Garatwa alisema ongezeko la mifugo katika maeneo yaliyoko pembezoni mwa hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni tishio kubwa kwa jamii na kuwa kuwepo mpango mahsusi ambao utanusuru migogoro ya kuvamia hifadhi.
Mwisho.



0 comments:

Post a Comment