Fahari ya Serengeti

Friday, November 25, 2016

UONGOZI WA KIJIJI CHA MOSONGO SERENGETI WAAHIDI KUWAKAMATA WATAKAOKEKETA WATOTO WA KIKE

Wakazi wa kijiji cha Mosongo kata Mosongo wilayani Serengeti wakifuatilia mada za athari za ukeketaji kutoka kwa wataalam wa Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti unaotekelezwa na amref health africa tanzania na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC).

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Itembe Makorere amesema hatakubali kukamatwa yeye kwa kuwalinda wanaokeketa watoto kinyume cha sheria ,bali watakuwa wa kwanza kutangulia polisi.

Amesema elimu iliyokwisha tolewa na makatazo ya vyombo vya dola kuwa ukeketaji ni kosa la jinai yeye kama kiongozi wa serikali hatawafumbia macho wale wote wanaoendesha vitendo vya ukeketaj






Wanafuatilia mada

Baadhi ya wazee wa mila wa kijiji cha Mosongo wakifuatilia mada,hata hivyo kundi hilo linalotajwa kuwa kinara wa ukeketaji kwa kutangaza tarehe,kuandaa ngariba na mamvo ya kiufundi lilitoa msimamo wake kuwa hawatahusuka na ukeketaji wa watoto wa kike bali watashughulika na tohara za watoto wa kiume.
Kamanda wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wilaya ya Serengeti Alfredy Kyebe akifafanua vifungu vinavyokataza ukeketaji na adhabu yake ambayo ni kifungo kisichopungua miaka mitano na isiyozidi miaka kumi na tano.
Meneja wa Mradi wa Tokomeza Ukeketaji Serengeti (amref)Godfrey Matumu akisisitiza jamii kujikita kuwasomesha watoto wa kike badala ya kuwakeketa kwa kuwa watoto wengi wanakataa kufanyiwa ukatili huo na baadhi wanakimbilia katika kituo cha nyumba salama .
Mtumishi wa Mungu Genya akifafanua vifungu vya biblia vinavyoharamisha ukeketaji .

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Mosongo Itembe Makorere amesema watakaompelekea kadi za sherehe za kukeketa watoto wa kike badala ya kuwapa zawadi atawakamata na kuwafikisha polisi kwa kuwa ni kosa la jinai kwa mjibu wa sheria .

Wanapika huku wakifuatilia mada
Balozi wa amref Christopher Genya akielezea umuhimu wa kusomesha mtoto wa kike kwa wakazi wa Mosongo.
Wanafuatilia.
Monica Nyeura kutoka kitengo cha Mama na Mtoto wilaya akitoa mada ya athari za ukeketaji kitabibu kwa niaba ya Mganga mkuu wa wilaya Salum Manyatta.

Wanafuatilia mada kwa makini
Joseph Mrimi mwenyekiti wa Ritongo akielezea umuhimu wa kusomesha watoto wa kike

Wanafuatilia.





0 comments:

Post a Comment