Fahari ya Serengeti

Friday, November 11, 2016

SERIKALI YAKUNJUA MAKUCHA DHIDI YA WAKEKETAJI



WAZAZI KIZIMBANI KWA KUKEKETA WATOTO WAO WATATU,
Anthony Mayunga,Mwananchi
amayunga@mwananchipapers.co.tz
Serengeti.Wazazi wawili wamepandishwa kizimbani kwa kosa la kuwakeketa watoto wao watatu kinyume cha kifungu cha 169(A)cha Sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Serengeti Amaria Mushi mwendesha Mashitaka wa Polisi Paschal Nkenyenge aliwataja washitakiwa kuwa ni Chacha Kiheta(35)na Mugusuhi Chacha(35)ambao ni mke na Mme wakazi wa kijiji cha Mesaga kata ya Kenyamota wilayani Serengeti wanadaiwa kuwakeketa watoto wao watatu kinyume cha sheria.
Aliimbia Mahakama kuwa washitakiwa kwa pamoja waliwakeketa watoto wao watatu wenye umri wa miaka (17),(16) na (13) desemba 21 mwaka 2015 kijijini hapo na kukamatwa novemba 10 mwaka huu,kwa kuwa kitendo hicho cha kikatili ni kinyume na kifungu cha 169(A)cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Hata hivyo washitakiwa baada ya kusomewa shitaka walikana kuwa si kweli ,kwa kuwa wao waliwakeketa watoto wao  mwaka jana si mwaka huu,wamepelekwa mahabusu baada ya kukosa wadhamini licha ya dhamana yao kuwa wazi.
Kesi hiyo ya  jinai  namba  210/2016 imeahirishwa  hadi novemba 24 mwaka huu  itakapotajwa tena .
Hivi karibuni katika mahakama hiyo ngariba Nyabitara Magori (45)na Nyakaho Msamba (64) bibi wa mtoto wakazi wa kijiji cha Mesaga walifikishwa katika mahakama hiyo kwa kosa la kumkeketa mtoto wa miaka (16)na kumsababishia dhara kuu,ambao wanaendelea kusota rumande baada ya kukosa wadhamini.
Serikali wilayani hapo imeishatoa agizo kwa watakaojihusisha na ukeketaji wakamatwe na kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili.
Mwisho.



0 comments:

Post a Comment