Fahari ya Serengeti

Monday, May 1, 2017

POLIS FC NA POLISI QUEENS MABINGWA WA MAKOMBE YA MEI MOSI

 Kamanda wa  Polisi wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara Mathew Mgema akiwa ameshikilia kombe baada ya timu ya Polisi Fc kuibuka bingwa wa kombe la Mei mosi kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Seronga Fc.
Pamoja na kombe wamepata sh 100,000 na mpira mmoja.
Timu ya mpira wa mikono wanawake ya Polisi nayo imeibuka bingwa baada ya kuifunga timu ya Chuo cha Uganga na uuguzi ya Kisare kwa mabao 12-2 na kupata kitita cha sh 50,000.


 Wanashangilia ushindi
 Tumeshindaaburudani hizo zimepamba maadhimisho ya mei mosi wilaya ya Serengeti
 Wachezaji wa timu ya mikono wanawake ya Polisi wakiwa wamepozi na kikombe chao kufuatia ushindi wa mabao 12-2 dhidi ya Kisare,Hongereni sana.

 Wanapongezana

 Mpambano wa mpira wa mikono wanawake,Kisare walikubali kupigishwa kwata na polisi kwa mabao 12-2.





 Kwaya ya walimu imekonga nyoyo wageni na wananchi ambao wamehudhuria maaadhimisho ya mei mosi na mkuu wa mkoa kuahidi kuitumia hiyo wakati wa ziara ya Rais mkoani humo.



 Skauti nao walikuwepo

Wageni wameshindwa kujizuia na kuamua kwenda kuserebuka.

0 comments:

Post a Comment