Fahari ya Serengeti

Wednesday, July 20, 2016

SERENGETI CULTURE FESTIVAL YAZINDULIWA

Mkurugenziwa Tanapa Allan Kijazi kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Serengeti Arts Group Paulina Boma wakati  akikagua mabanda ya wajasiliamali,taasisi za umma na binafsi wakati wa tamasha la Serengeti Culture Festival lililoandaliwa na Serengeti Culture Centre kwenye viwanja vya Right To Play mjini Mugumu wilayani Serengeti.
Baadhi ya watazamaji wakiwa juu ya mti wakifuatilia burudani mbalimbali zinazotolewa ndani ya eneo la michezo wakati wa tamasha la Serengeti Culture Festival.
Kijazi akikagua banda la Senapa.
Anatia sahihi kuthibitisha alifika kwenye banda hilo wakati wa tamasha hilo ambalo linajumuisha watu kutoka kona zote za nchi ya Tanzania ikiwemo vikundi vya burudani.
Hilo ni Banda la Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ambao wanashiriki katika maonesho hayo ikiwa ni pamoja na kuelezea kazi wazifanyazo kwa jamii .
Akikagua banda la Takukuru wilaya ya Serengeti.
Analakiwa na mratibu wa Nyumba Salama Rhobi Samweli ambao licha ya kuwahifadhi watoto waliokimbia kukeketwa pia huwafundisha kazi mbalimbali za mkono na baadhi ya kazi hizo ndizo zimewasilishwa kwenye maonesho hayo.
Burudani zilikuwepo ,kikundi kutoka Butiama kilikuwa kivutio.
Mzunguko kwenye vibanda unaelekea mwisho.
Burudani,burudani ,burudani.
kazi inaenda ikiongezeka

Katibu Tawala wilaya ya Serengeti Cosmas Qamara akisisitiza jambo kwa wananchi kuhusu umuhimu wa tamasha hilo la kitamaduni.
Ilipofika wakati wa hotuba alisisitiza matumizi ya mila na desturi zilizo nzuri kwa ajili ya kukuza utalii wa ndani na nje.

Anasisitiza.
Ukaguzi unaendelea.

0 comments:

Post a Comment