Fahari ya Serengeti

Saturday, July 23, 2016

DC Serengeti atoa siku tano chanzo cha maji cha zamani kianze kutoa huduma ya maji kwa hospitali na kwa jamii wakati wanarekebisha mfumo wa umeme manchira

 Dc Serengeti Nurdin Babu atoa siku tano kwa Mamlaka na idaraya maji kufufua chanzo cha zamani cha maji ili kianze kutoa huduma hospitali na kwa jamii wakati wanaendelea na marekebisho ya mfumo wa umeme kwenye pampu ya maji bwawa la Manchira.
Kwa mjibu wa agizo hilo lililotolewa julai 21 mwaka huu katika kikao cha pamoja na Ded na wataalam wa idara hiyo utekelezaji wake unatakiwa kukamilika julai 26 iwapo watashindwa kukamilisha hatua kali dhidi yao zitachukuliwa.
Ikimbukwe kabla ya chanzo cha bwawa la manchira mji wa mugumu na viunga vyake vilikuwa vikipata huduma ya maji kutoka kwenye vyanzo hivyo kwa kutumia mashine za dizeli na wakati na nyingine waliweka sola.




0 comments:

Post a Comment