Fahari ya Serengeti

Thursday, July 7, 2016

KAZI YA KUFUNGA PAMPU BWAWA LA MANCHIRA IMEKAMILIKA NA SASA MAJI YAANZA KUTOKA MJINI

 Mafundi kutoka Muwasa na Muguwasa wakiwa kwenye mtumbwi wakisafirisha Pampu kuelekea eneo la kufunga katika bwawa la Manchira wilayani Serengeti,kazi hiyo ilifanyika kwa siku mbili hatimaye na kufaulu kuwasha mashine na maji kuanza kutoka katika baadhi ya maeneo Kwa zaidi ya miezi miwili mji huo ulikuwa unakabiliwa na tatizo la maji kufuatia Pampu hiyo kuungua na kulazimu wananchi kuchota maji kwenye visima mbalimbali,huku bei ya maji ikipanda kutoka sh 100 hadi 500 kwa dumu moja.
 Maandalizi ya kutandaza nyaya kwa ajili ya kufunga kwenye pampu yakiwa yanaendelea kama inavyoendelea.
 Kazi haikuwa rahisi kutokana na uzito wa pampu hiyo na nyenzo duni ,hapo wanaisogeza bwawani.
 Wakati mwingine walilazimika kushaurina njia za kufanya ili kuifikisha pampu eneo husika ambalo liko ndani ya bwawa na pana kina kirefu cha futi 8 hadi 9.
 Kazi ya kufunga inaendelea.
 Mtumbwi wa kienyeji umeandaliwa kwa ajili ya kusafirisha Pampu.

 Kuna haja ya kufanya usafi karibu na chanzo cha maji ili mazingira yawe safi.
 Kazi ya kusogeza pampu ilishirikisha kila mmoja hapo.


 Kazi ya kuinganisha kabla ya kwenda kuifunga ilifanyika.
 Ubunifu ulitumika wa namna ya kusafirisha pampu hiyo kama inavyoonekana.
 Kazi ya kupeleka pampu kwenye mtumbwi inaendelea.
 Baadhi ya mafundi wakiwa wanachunguza mtumbwi kabla ya kuweka pampu.


 Kazi inaendelea

 Safari inaendelea ingawa ilikuwa ni hatari kutokana na mtumbwi wa kienyeji walioutumia,na wakati mwingine chuma kilichokuwa kikitumika kama podo kuwa kifupi na kukosa mwelekeo.


 Hapo ilimlazimu mmoja wa mafundi kumsaidia nahodha
 Pamoja na mafundi kutumia mbinu mbalimbali kwenda eneo la kazi,hata hivyo ilishindana na kuishia njia kama inavyoonekana.
 Safari inaendelea huku baadhi wakishuhudia nini kitatokea.
 Nahodha kuna wakati aliteleza na kuanguka majini na kumlazimu mmoja wa mafundi kusaidia kuongoza mtumbwi huku yeye akitumia uzoefu wake kuogelea .





Life Jacket ziliwasaidia wengine kuogelea.

0 comments:

Post a Comment