Fahari ya Serengeti

Thursday, May 26, 2016

MAJI NA SUKARI PASUA KICHWA KWA WAKAZI WA MJI WA MUGUMU SERENGETI

MAJI SUKARI YAWATESA WAKAZI WA MJI WA MUGUMU
SERENGETI MEDIA CENTRE
Wakazi wa Mji wa Mugumu wilayani hapa Mkoa wa Mara wanakabiliwa na ukosefu wa maji safi kwa zaidi ya wiki mbili kufuatia mtambo wa kusukuma maji kutoka bwawa la Manchira kuungua.
Wakati sukari ikiuzwa  kati yash 3000-hadi 3500 kwa kilo na ikitolewa Nchini Kenya kwa njia za panya,ndoo ya maji imepanda kutoka sh  100 kwa maji ya bomba hadi sh 500 kwa maji ya shimoni na visima ,hali ambayo inazidisha makali ya maisha kwa wananchi na ni tishio la ongezeko la magonjwa yanayosababishwa na maji..
Baadhi ya wakazi wa mji huo walisemalicha ya maji waliyokuwa wanapata kutoka bwawa la Manchira kutokutibiwa  lakini yalikuwa yanapatikana kwenye mabomba kwa wakati wote na kwa gharama nafuu,ukilinganisha na hali ilivyo sasa ambapo wengi wanalazimika kuamka alfajiri kwenda kutafuta kwenye visima vya watu.
Meneja wa Mamlaka ya Maji Mugumu Dickson Kasese akiongea na Serengeti Media Centre kwa njia ya simu   alidai kuwa mtambo wa kusukuma maji umeungua kutokana na hitilafu ya umeme na kuwa zinatakiwa zaidi ya sh 180 mil za kununua mwingine.
“Inahitajika Pampu mpya maana Control Panel,Cable ya kuendesha motor zote zimekufa,tatizo hilo limebebwa na Mamlaka ya Maji Musoma ,na mtambo huo hapa nchini hakuna wameagiza nje ,itachukua zaidi ya wiki nne,tunatarajia mwishoni mwa mwezi juni au mwanzoni mwa julai  kama hatutapata njia  nyingine ya dharura,”alisema.
Alisema kwa sasa yuko Dar es Salaam wizara ya Maji ili kuwasilisha ombi la kupata mtambo mwingine utakaosaidia kutoa huduma kwa wananchi,hata hivyo alisema maelezo yao yanadai kuwa hawana mpaka waagize  nje na hautapatikana kwa muda mfupi kwa kuwa mpaka watengenezewe kiwandani.
Consolatha John,Esther Magige wakazi wa mtaa wa NHC mjini Mugumu walisema kuwa maji wanayouziwa kwa  sh 500 ni ya kwenye madimbwi ambayo yametuama wakati wa mvua,hivyo kama tatizo hilo halitapata ufumbuzi wa haraka huenda kukaibuka magonjwa ya mlipuko chanzo kikiwa maji.
Baadhi ya taasisi zilizokwishaanza onja adha ya ukosefu wa maji ni  pamoja na hospitali Teule ya Nyerere,gereza mahabusu,Kituo cha Nyumba Salama ,Machinjio  na wafanyabiashara wa nyumba za kulala wageni,migahawa na hoteli ambazo zilitegemea maji ya bomba kutoka bwawa la Manchira.
Hata hivyo baadhi ya wauza maji walisema kwa sasa wanapata faida kubwa nakudai kama matengenezo yatachukua muda mrefu wanategemea bei ya maji itapanda kwa kuwa hitaji litakuwa kubwa.
Mwisho.


 Baadhi ya wakazi wa Mtaa Mwema mjini Mugumu wakichota maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali katika kisima cha Chakuburya,






 Baadhi wa kazi wa mji wa Mugumu wakichota maji kwenye mtaro wa barabara eneo la Mkuu wa wilaya kwa ajii ya matumizi ya nyumbani,maji hayo ambayo si safi na salama.


0 comments:

Post a Comment