Fahari ya Serengeti

Saturday, May 21, 2016

ZAIDI YA SH 111 MILIONI ZACHANGWA KUTENGENEZA MADAWATI SERENGETI


 
Serengeti Media Centre.
Zaidi ya sh 111 milioni zimechangwa na wadau mbalimbali wa maendeleo wilayani hapa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kutatua changamoto ya upungufu wa madawati 16,000 kwa shule za Msingi na Sekondari.
Michango hiyo imetolewa na wadau wa maendeleo wakati wa kikao cha kuweka mikakati ya namna ya kutatua changamoto ya ukosefu wa madawati kwa shule za Msingi na sekondari ,ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Dk John Magufuli la kuhakikisha tatizo la madawati linakwisha kufikia juni 30 mwaka huu kwenye ukumbi wa Giraffe Garden mjini hapa.
Mkuu wa wilaya hiyo Maftah Ally alisema baada ya kuguswa na matatizo yanayowakabili wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na kuamua kuchangia fedha taslimu 3,313,000,ahadi za fedha sh 50,540,000 na ahadi ya madawati 477 kutoka kwa wadau mbalimbali.
“Kikao hiki kilikuwa cha kuweka mikakati ya kupata sh 2 bilioni kwa kupata madawati 14,594 kwa shule za msingi,meza 2,259 na viti 2,689 kwa shule za sekondari , wadau baada ya kuona ukubwa wa tatizo wakaamua kuchangia kiasi hicho,”alisema.
Mbunge wa jimbo hilo Mwalimu Marwa Ryoba aliyechangia madawati 100 yenye thamani y ash 12 mil,alisema shule nyingi zinakabiliwa na matatizo ya ukosefu wa madawati,hali ambayo inachangia kushuka kwa taaluma na ufaulu.
“Ofisi yangu imetoa imetoa madawati 100 kwa kuanzia na tutaendelea kuchangia ili tuhakikishe watoto wetu hawakai chini,na kitakachofuata ni vyumba vya madarasa,baada ya hapa tutawaunganisha wana Serengeti waioshio nje ya mkoa huu waweze kuchangia maendeleo ya wilaya yao,”alisema.
Mhifadhi wa Ujilani Mwema wa hifadhi ya Taifa ya Serengeti Nuhu Daniel alisema Tanapa imetoa sh 154 mil kwa wilaya nane zinazopakana na hifadhi hiyo na kila moja imepata zaidi ya sh 18 mil kwa ajili ya madawati,”pia tumetengeneza madawati 30 kwa ajili ya shule ya msingi Fort Ikoma,na tutaendelea kusaidia jamii inayotuzunguka kama ilivyo sera yetu,”alisema.
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Juma Porini alisema halmashauri yake imetenga sh 100 milioni kwa ajili ya kutengeneza madawati,hivyo mchango huo wa wadau utasaidia kupunguza ukubwa wa tatizo na kuwataka wadau wanaowazunguka  washirikiane kusukuma mbele maendeleo ya wilaya hiyo.
Mkurugenzi wa Kibo  Safari’s Willy Chamburo ambaye anaendesha biashara ya utalii maeneo mbalimbali ikiwemo Serengeti alichangia madawati 50 yenye thamani ya Sh 6 milioni na kuwataka wafanyabiashara wa wilaya hiyo kuhakikisha wanashimana ili kuwajengea mazingira mazuri ya maisha watoto wao.
Baadhi ya wadau mbalimbali waliochangia ni pamoja wawekeza wa sekta ya utalii,wafugaji,wasanii,bodaboda,wakulima,Serengeti Media Centre,Ikona Wmas ,wafanyabiashara,Benki za Nmb,Crdb,Posta  na watumishi wa idara mbalimbali za umma.
Wilaya hiyo ina shule za msingi 110 za serikali zenye jumla ya wanafunzi 76302,sekondari 21 zenye wanafunzi 9359,inakabiliwa na upungufu wa madawati 14,594 kwa shule za msingi na sekondari meza 2259 na viti 2,689.
Mwisho.

 Igizo la kikundi cha Nyota Njema liliwakonga nyoyo wadau waliohudhuria kikao cha kuweka mikakati ya maendeleo ambacho kilizaa harambee ya zaidi ya sh 111 milioni.






 Mnada wa ng'ombe ulifanyika kwa ajili ya kukusanya fedha za utengenezaji wa madawati


 mijadala mbalimbali inaendelea nje ya Ukumbi

 Mnada wa Dvd ulifanyika ili kukusanya fedha za madawati





















Dc Maftah Ally akitoa taarifa ya makusanyo na nini kitaendelea baada ya hapo ili kuhakikisha wanakamilisha kazi ya madawati

0 comments:

Post a Comment