Fahari ya Serengeti

Tuesday, March 31, 2015

ANAHITAJI MSAADA



| Na Serengeti Media Centre
Godfrey Msagati(23)mkazi wa Mugumu wilaya ya Serengeti anahitaji msaada wa pesa ili aende Oceon Road kwa matibabu ya Kansa ,hapo yuko na mama yake mzazi,picha na Serengeti Media Centre

Posted  Ijumaa,Marchi27  2015 
Kwa ufupi
Nashon mzaliwa wa Mugumu Wilaya ya Serengeti kwa kipindi cha miaka saba, alikuwa akifanya kazi na kampuni moja ya Kichina iliyopo nchini.
Geofrey Msagati (23), ni Fundi Seremala ambaye ndoto za siku moja kufungua kampuni yake zimezimika na wala hajui hatima ya maisha yake kutokana na maradhi yanayomsibu.
Nashon mzaliwa wa Mugumu Wilaya ya Serengeti kwa kipindi cha miaka saba, alikuwa akifanya kazi na kampuni moja ya Kichina iliyopo nchini.
Kampuni hiyo ilishiriki kujenga majengo mbalimbali nchini ikiwamo Hoteli ya Kiwanda cha Saruji cha Kigamboni pamoja na hoteli kadhaa za kitalii Zanzibar na Mtwara, pia nyumba za wafanyakazi wa mradi wa gesi Mtwara.
Kwa sasa ‘yupo gizani’ kutokana sehemu kubwa ya maisha yake kuitumia akiwa kitandani.
Hali hiyo kwa Msagati ambaye ni mkazi wa Mtaa wa NHC mjini Mugumu, mkoani Mara inatokana na maradhi yanayoelezwa kuwa ni saratani iliyosababisha mguu wake kuvimba tangu unyayo hadi pajani, hata kushindwa kutembea wala kuvaa nguo.
Anaeleza kwamba alikutwa na mkasa huo alipokuwa kazini, wakati akiweka ‘jipsum’ katika moja ya nyumba za wafanyakazi wa mradi wa gesi Mtwara.
“Machi mwaka jana nikiwa na wenzangu mkoani Mtwara katika ujenzi wa nyumba za wafanyakazi wa mradi wa gesi, mguu wangu uliteleza kutoka mbao nilizokuwa nimekanyaga na moja ikanigonga mguuni eneo la ugoko… nilihisi maumivu makali, lakini baadaye nikaendelea na kazi,” anasimulia Msagati huku akiugulia maumivu.
Anasema siku hiyo aliendelea na kazi bila kujua kama madhara yake yatakuwa kama yalivyo sasa, lakini bahati mbaya mwajiri wangu hakutaka nikachunguze afya yangu.
“Kumbe walinihitaji mimi kwa utaalamu wangu, wala hawakujali afya yangu…. sasa nakufa huku nakijiona na hakuna msaada wowote kutoka kwao,” anasema huku akitokwa na machozi.
Msagati anaeleza kuwa matibabu aliyokuwa akipata ni dawa za maumivu, huku akiendelea na kazi na kwamba hata alipoomba fedha kwa ajili ya matibabu hakupewa na kulazimika kujitibu na baadaye akapewa nauli ya kumrudisha Dar es Salaam.
Anaeleza kuwa akiwa huko alipata huduma na dawa za maumivu hali ikawa nzuri na kurejea Zanzibar kwenye ujenzi wa hoteli moja ya kitalii.
“Nikiwa Zanzibar maumivu yalianza tena nikaenda Hospitali ya Mnazi Mmoja, nikapigwa X-ray wakasema nyonga na mifupa iko sawa na kwamba huenda ni mishipa haijakaa vizuri. Nikapewa dawa za maumivu, lakini hali ikazidi kuwa mbaya ndipo nikarudishwa Dar es Salaam bila msaada,” anasema.
Anaeleza kuwa alirudishwa Dar es Salaam huku akitembea kwa kuchechemea kutokana na maumivu, ndipo Oktoba mwaka 2014 alipoona hali inazidi kuwa mbaya aliomba atumiwe nauli na mama yake ili aweze kurudi nyumbani.
Msagati anasema Desemba mwaka jana mguu wake ukaanza kuvimba huku uwezo wa kutembea ukipungua. Alikwenda Hospitali Teule ya Nyerere, Wilaya ya Serengeti ambako madaktari walimpa rufaa kwenda KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro kwa mabingwa wa mifupa.
“Hatukwenda kwa wakati kwa kuwa mama alikuwa ameishiwa fedha. Ikabidi mama aanze kazi ya kuomba kwa msaada kwa watu mbalimbali na makanisani. Tulipopata fedha Februari mwaka huu, nikapelekwa KCMC na madaktari walisema nina saratani kwenye mifupa, hivyo nipelekwe Taasisi ya Saratani Ocean Road Dar es Salaam,” anasema Msagati na kuongeza:
“Tatizo ni fedha maana naishi na mama ambaye anafanya biashara ndogondogo. Kuna wadogo zangu wanasoma, naye kwa kipindi chote hafanyi kazi maana ndiye anayenibeba kila hatua, kampuni niliyofanya kazi haijanisadia wala haikutaka kutupatia mikataba ya kazi, hivyo nashindwa nianzie wapi.”
Kilio cha mama
Mama wa Msagati, Lucy Magere anasema anachokiomba kwa sasa kutoka kwa Watanzania ni kunusuru maisha ya kijana wake kwa kuwa hana uwezo wala namna ya kufanya kutokana na umaskini huku akiishi kwa misaada ya watu wanaofika kumjulia hali mgonjwa.
“Kwa kipindi chote niko ndani namhudumia Msagati, sina muda wa kutoka hata kufanya ujasiriamali, mtaji wenyewe umeisha… maana hivi nililazimika kukaa hospitali kwa muda mrefu kutokana na hali yake kuwa mbaya,” anasema.
Anaomba wanaoguswa wamsaidie huku akiishauri Serikali kufuatilia kampuni za kigeni kwa kuwa hazitoi mikataba kwa wafanyakazi wake na wanapopata matatizo haziwasaidii.... “Kijana wangu kakaa na kampuni kwa miaka saba, lakini ameugua wamemtekeleza na mimi ndiyo nahangaika.”
Msagati anasema licha ya kuugua, mabosi wake hao huwa wamampigia simu mara kwa mara wakimtaka arudi kazini.
Kwa watakaoguswa wawasiliane kwa simu namba 0787 337562 au 0768522546.





0 comments:

Post a Comment