Fahari ya Serengeti

Friday, November 18, 2016

KANISA LA AGAPE WUEMA SANCTUARY MINISTRIES KUJENGA HOSPITALI YA RUFAA NA CHUO MUSATI SERENGETI

Diwani wa kata ya kibanchabanche Philemon Chacha(wa pili kushoto)akimuonyesha Askofu mkuu wa Kanisa la Agape Martin Gwila(kushoto) eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Hospital ya Rufaa.
Viongozi wakuu kutoka kanisa la Agape Wuema Sactuary Ministries International wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu(wa pili kushoto mstari wa mbele)mara baada ya mazungumzo yalifanyika katika ofisi ya mkuu wa wilaya.
Mwenyekiti wa kijiji cha Musati Daudi Mgendi(aliyenyoosha mkono)akitoa maelekezo kwa viongozi wa kanisa la Agape mara baada ya kuwasili katika eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Hospital.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Agape Martin Gwila(wa pili kushoto)akiteta jambo na baadhi ya viongozi mara baada ya kuwasili katika eneo la ujenzi wa Hospital ya Rufaa katika kijiji cha Musati.


Waendesha pikipiki almaarufu kama bodaboda wakiongoza msafara wa Viongozi kwenda kuangalia eneo la ujenzi wa Hospitali katika kijiji cha Musati.


Viongozi wa Dini na viongozi wa Serilaki wakiwasili katika shule ya msingi Musati kwa ajili ya kuongea na wananchi wa kijiji hicho mara baada ya kupokea eneo walilopewa kwa ajili ya ujenzi.
Baadhi ya Viongozi na wananchi wakikagua mradi wa Maji katika kijiji cha Musati.
Askofu Martin Gwila Akipongezana na mkewe Agness Martin mara baada ya kupokea eneo lenye takribani ekari 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospital ya Rufaa.
Diwani wa Kata ya Kebanchabanche Phillemon Chacha akisalimiana na wananchi wake katika mkutano uliofanyika shule ya msingi Musati.
Maaskofu wa Kanisa la Agape Wuema Ministry wakifanya mazungumzo na Katibu Tawala wilaya ya Serengeti Donald(wa nne kushoto) Kamara mara baada ya kuwasili ofisini kwake.
Diwani kata ya Kebanchabanche Philemon Chacha akitoa utambulisho kwa wananchi kuhusiana na ugeni uliowasili kijijini hapo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Musati Daudi Mgendi akiwashukuru wananchi wake wakioudhuria kikao cha makabidhiano ya kiwanja kwa viongozi wa kanisa la Agape Wuema Ministry.


Askofu Mkuu wa Agape Wuema Ministry Martin Gwila akitoa Shukurani kwa wananchi wa kijiji cha Musati mara baada ya kupokea eneo kwa aijili ya ujenzi wa Hospital ya Rufaa.
Wananchi wa kijiji cha Musati wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wakuu wa Dini kutoka kanisa la Agape Wuema katika mkutano uliofanyika shule ya msingi Musati.
Askofu Godmon kutoka mkoani Morogoro akifanya maombezi kabla ya kuanza kwa mkutano na wananchi wa kijiji cha Musati kata ya Kebanchabanche.
Askofu Martin Gwila akifurahi mara baada ya kukabidhiwa Zawadi ya Mbuzi kutoka kwa wazee wa Mila kijiji cha Musati kata ya Kebanchebanche.
Mzee wa Mila Kisamarwa(wa pili kushoto) akimkabidhi Askofu Martin Gwila zawadi ya Mbuzi kwa niaba ya wazee wa mila wa kijiji cha Musati.


0 comments:

Post a Comment